Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI
Admin.Frank Mugogo 536

REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri amepongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kupanda miti zaidi ya 2000 katika Hospitali ya Taifa ya Magonjwa ya Akili ya Milembe.

Akizungumza wakati wa zoezi la upandaji wa miti hiyo lililofanyika tarehe 4 Mei 2022 katika viwanja vya Hospitali ya Milembe ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, Mhe. Shekimweri alisema kuwa ni wajibu wa wadau wote kuhakikisha miti hiyo inaota vizuri na kuwa itachangia kuweka mandhari nzuri inayoweza kuvutia utalii wa mazingira.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Masoko na Teknolojia wa REA, Mhandisi Advera Mwijage alihimiza utunzaji wa mazingira ili kuendelea kutunza vyanzo vya maji na kuweza kupata mvua za kutosha.

Naye Mkuu wa Idara ya Mazingira ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Dodoma ya Kijani inawezekana kwa kuendelea kupanda miti na kuitunza ili iote na alitoa wito kwa wakazi wa Dodoma kupanda miti ya kivuli pamoja nay a matunda kwa ajili ya kutunza mazingira.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«May 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2829301234
567891011
12131415
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Read more
16
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Read more
1718
19
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Read more
202122
Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 20 wa kusambaza umeme katika vitongoji 180 utakaonufaisha zaidi ya Kaya 5,940 Mkoani Tanga.

Read more
232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top