Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Atembelea Maonesho ya Wizara ya Nishati
Admin.Frank Mugogo 654

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Atembelea Maonesho ya Wizara ya Nishati

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson amewashauri Waheshimiwa Wabunge kutumia fursa ya Maonesho ya majukumu ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kupata taarifa za utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini katika maeneo yao.

Mhe. Ackson alitoa ushauri huo alipotembelea Maonesho hayo ya siku tatu yaliyoanza tarehe 23 Mei, 2022. “Tumepata fursa hapa ya kujua vijiji vingapi havijafikiwa umeme na vijiji vingapi vimefikiwa na huduma hiyo, wizara inajipanga kuelekea kwenye vitongoji. Kwa hiyo vitu kama hivyo ni vizuri, sasa Waheshimiwa Wabunge wamepata nafasi na wanaendelea kupata nafasi kwa sababu leo ni siku ya kwanza” alisema.

Awali, Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba alisema lengo la Maonesho hayo ni kuwawesha Waheshimiwa Wabunge kupata majibu ya maswali waliyonayo kuhusu Wizara na Taasisi zake pamoja na huduma zinazotolewa.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Mhe. Sebastian Kapufi aliipongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa kazi nzuri katika miradi ya kusambaza umeme vijijini na kuwa amepata majibu ya changamoto za maeneo y Jimbo lake. “Nilikuwa na shida katika Kata za Mwampulu na Kasokola wamepeleka nguzo, nasubiri tuu mwezi ujao mambo yaende kwa kasi” alisema Mbunge huyo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top