Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Atembelea Maonesho ya Wizara ya Nishati
Admin.Frank Mugogo 641

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Atembelea Maonesho ya Wizara ya Nishati

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson amewashauri Waheshimiwa Wabunge kutumia fursa ya Maonesho ya majukumu ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kupata taarifa za utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini katika maeneo yao.

Mhe. Ackson alitoa ushauri huo alipotembelea Maonesho hayo ya siku tatu yaliyoanza tarehe 23 Mei, 2022. “Tumepata fursa hapa ya kujua vijiji vingapi havijafikiwa umeme na vijiji vingapi vimefikiwa na huduma hiyo, wizara inajipanga kuelekea kwenye vitongoji. Kwa hiyo vitu kama hivyo ni vizuri, sasa Waheshimiwa Wabunge wamepata nafasi na wanaendelea kupata nafasi kwa sababu leo ni siku ya kwanza” alisema.

Awali, Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba alisema lengo la Maonesho hayo ni kuwawesha Waheshimiwa Wabunge kupata majibu ya maswali waliyonayo kuhusu Wizara na Taasisi zake pamoja na huduma zinazotolewa.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Mhe. Sebastian Kapufi aliipongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa kazi nzuri katika miradi ya kusambaza umeme vijijini na kuwa amepata majibu ya changamoto za maeneo y Jimbo lake. “Nilikuwa na shida katika Kata za Mwampulu na Kasokola wamepeleka nguzo, nasubiri tuu mwezi ujao mambo yaende kwa kasi” alisema Mbunge huyo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top