Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI
Admin.Frank Mugogo 877

REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri amepongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kupanda miti zaidi ya 2000 katika Hospitali ya Taifa ya Magonjwa ya Akili ya Milembe.

Akizungumza wakati wa zoezi la upandaji wa miti hiyo lililofanyika tarehe 4 Mei 2022 katika viwanja vya Hospitali ya Milembe ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, Mhe. Shekimweri alisema kuwa ni wajibu wa wadau wote kuhakikisha miti hiyo inaota vizuri na kuwa itachangia kuweka mandhari nzuri inayoweza kuvutia utalii wa mazingira.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Masoko na Teknolojia wa REA, Mhandisi Advera Mwijage alihimiza utunzaji wa mazingira ili kuendelea kutunza vyanzo vya maji na kuweza kupata mvua za kutosha.

Naye Mkuu wa Idara ya Mazingira ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Dodoma ya Kijani inawezekana kwa kuendelea kupanda miti na kuitunza ili iote na alitoa wito kwa wakazi wa Dodoma kupanda miti ya kivuli pamoja nay a matunda kwa ajili ya kutunza mazingira.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«June 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
12
Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.

Read more
34567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top