Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI
Admin.Frank Mugogo 401

REA WAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri amepongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kupanda miti zaidi ya 2000 katika Hospitali ya Taifa ya Magonjwa ya Akili ya Milembe.

Akizungumza wakati wa zoezi la upandaji wa miti hiyo lililofanyika tarehe 4 Mei 2022 katika viwanja vya Hospitali ya Milembe ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, Mhe. Shekimweri alisema kuwa ni wajibu wa wadau wote kuhakikisha miti hiyo inaota vizuri na kuwa itachangia kuweka mandhari nzuri inayoweza kuvutia utalii wa mazingira.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Masoko na Teknolojia wa REA, Mhandisi Advera Mwijage alihimiza utunzaji wa mazingira ili kuendelea kutunza vyanzo vya maji na kuweza kupata mvua za kutosha.

Naye Mkuu wa Idara ya Mazingira ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Dodoma ya Kijani inawezekana kwa kuendelea kupanda miti na kuitunza ili iote na alitoa wito kwa wakazi wa Dodoma kupanda miti ya kivuli pamoja nay a matunda kwa ajili ya kutunza mazingira.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top