Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wananchi waaswa kutunza mazingira
Frank A. Mugogo 386

Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewaasa wananchi kutunza mazingira na kulinda miundombinu pamoja na vyanzo vya maji ili kuendelea kupata huduma ya umeme pamoja na kuwa na miradi endelevu ya kufua umeme. 

Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage ametoa rai hiyo Wilayani Ludewa Agosti 27, 2024 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya matengenezo ya mitambo ya kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji ya mradi wa Lugarawa. 

Mradi wa Lugarawa unasimamiwa na Kampuni ya Madope na unamilikiwa kwa ushirikiano baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe, Watumia Umeme Ludewa (wananchi) na Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa. 

Mhandisi Advera alifafanua kuwa mradi unatumia Nishati Safi na Salama kutokana na maporomoko ya maji hivyo ili mradi uwe endelevu wananchi washirikiane kutunza mazingira. 

Akizungumzia dhumuni la ziara yake katika mradi, Mhandisi Advera alisema mradi huo wa Madope ni miongoni mwa miradi ya kufua umeme kwa kutumia Nishati Jadidifu inayowezeshwa na REA. 

"Nimefika hapa kukagua shughuli zinazoendelea za matengenezo ya mitambo, kama mnavyotambua REA inawezesha miradi hii; kuna fedha ya Serikali hapa; hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha kila kitu kinakwenda vizuri na kuhakikisha uzalishaji unaendelea," alifafanua. 

Alisema zaidi ya wateja 5,000 walikuwa wanahudumiwa na mradi lakini tangu umesimama kutokana na hitilafu iliyojitokeza wateja hao kwa sasa wanahudumiwa na TANESCO kupitia miundombinu ya usambazaji iliyojengwa na REA. 

Alisema mara baada ya matengenezo kukamilika; umeme utakaozalishwa na mradi utaingizwa katika Gridi ya Taifa kupitia miundombinu iliyopo. 

Kwa upande wake Meneja wa Mradi, Mhandisi Masanja Kurwa alisema mradi uliwezeshwa na REA na kwamba ulianza rasmi kuzalisha umeme tarehe 30 Agosti, 2019 ambapo ulikuwa ukihudumia Vijiji 20 katika Kata 6 Wilayani humo. 

Alisema mradi ulisanifiwa kuzalisha Kilowat 1,700 lakini haukuweza kufikisha na hivyo Serikali ilielekeza kusimamisha uzalishaji ili kufanya maboresho ya mitambo ili kufikia lengo. 

"Tunaishukuru REA kwa kuendelea kutushika mkono tangu hatua za awali kabisa za ujenzi na hata sasa katika haya maboresho tunayofanya tayari tumepewa fedha na REA na sasa tunasubiri Mkandarasi akamilishe ili tuuze umeme kwa TANESCO," alisema Mhandisi Kurwa. 

Mhandisi Kurwa amesema wanamtarajia Mkandarasi ambaye ni Kampuni ya ZECO mwenye makao makuu yake Nchini Italia kufika hapo kwa ajili ya maboresho na kwamba taratibu zingine zimekamilika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top