Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yatoa Mafunzo ya Nishati Safi kwa Makundi Maalum
Frank A. Mugogo 159

REA Yatoa Mafunzo ya Nishati Safi kwa Makundi Maalum

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imepongezwa kwa kuwezesha na kuhamasisha upatikanaji wa  nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji ili watanzania watumie nishati safi na salama nchini.

Pongezi hizo zimetolewa leo Oktoba 23, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mhe. Jamila Yusuf wakati akifungua mafunzo ya elimu ya matumizi ya nishati safi kwa Makindi Maalum iliyofanyika mkoani Katavi.

Mhe. Yusuf amewapongeza pia TAMAVITA (Taasisi ya Maendeleo kwa Viziwi Tanzania) kwa kushirikiana na REA katika uhamasishaji na kukubali kupewa mafunzo hayo kutoka REA ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Ameongeza kuwa, Rais Samia ni kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini na kuwapongeza TAMAVITA kwa kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhama kutoka kwenye matumizi ya nishati zisizo safi na salama na kuanza kutumia nishati safi ya kupikia.

Amesema matumizi ya nishati zisizo safi zinamadhara kwa afya ya binaadamu kupitia joto na moshi unaotokana na nishati hizo ambao unatoa kemikali ambayo sio salama kwa afya hivyo kila mmoja abadilike na amhamasishe mwingine katika hilo.

Naye, Mhandisi kutoka REA, Ramadhan Mganga amesema kuwa Wakala umeandaa mpango maalum wa kuwezesha taasisi zinazoandaa chakula na kulisha watu zaidi ya 100 kwa siku  kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia.

"Tunataka ifikapo mwaka 2034; 80% ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia, kwa manufaa yao na vizazi vijavyo," amesisitiza Mha. Mganga.

Kwa upande wake, Meneja wa Bishara kutoka Tango Energy Limited, Sunday Nyembele amesema kuwa jumla ya majiko banifu 60 yatauzws kwa TAMAVITA katika semina hiyo na majiko banifu 3,126 yatauzwa kwa wananchi wa mkoa wa Katavi.

TAMAVITA ni taasisi maalum kwa walemavu wasiosikia viziwi inayojushughulisha na shughuli za ujasiliamali pamoja na utoaji wa elimu mbalimbali katika jamii ya walemavu viziwi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
1718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top