Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Serikali Imetoa Shilingi Billioni 50 kwa Waendelezaji Wadogo Wadogo wa Miradi ya Nishati Jadidifu
Admin.Frank Mugogo 6714

Serikali Imetoa Shilingi Billioni 50 kwa Waendelezaji Wadogo Wadogo wa Miradi ya Nishati Jadidifu

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa takribani Shilingi Bilioni 50 kwa ajili ya kuwawezesha waendelezaji wadogo wadogo kwenye miradi ya nishati jadidifu katika maeneo yaliyopo vijijini Tanzania Bara.

Nishati hizo ni pamoja na umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vya jua, upepo, maporomoko madogo ya maji pamoja na tungamo taka. Fedha hizi zimetolewa kufanikisha kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa taarifa za awali za mradi (upembuzi yakinifu), mpango biashara pamoja na taarifa za mazingira. Pia fedha zimetolewa kwa ajili ya kuunganisha wateja wakati wa utekelezaji wa mradi pamoja na kuwakopesha waendelezaji hao kwa ajili ya ujenzi wa miradi hiyo.

Akifungua kikao cha pili kati ya Wizara ya Nishati, REA, TANESCO, EWURA na Waendelezaji hao kilichofanyika Septemba 19, 2019 katika ukumbi mdogo wa Bunge jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nishati Mh. Dkt. Merdad Kalemani (Mb) alisema Serikali inatambua mchango wa waendelezaji hao wa nishati ambao hadi sasa wamezalisha umeme wa takribani 17MW ambao umeingizwa katika gridi ya Taifa na mwingine kuwauzia moja kwa moja wananchi wa vijijini. Mh. Waziri alisema kuna dola za Marekani Milioni 54.5 kwa ajili ya kuwawezesha wawekezaji binafsi. Fedha hizi zimetengwa kwa Mwaka wa Fedha 2019/20. Aidha Dr. Kalemani alisisitiza kuwa, Serikali imeweka lengo la kuzalisha umeme wa 10,000MW ifikapo Mwaka 2025, hivyo anategemea waendelezaji binafsi wachangie katika uzalishaji huu ili kufikia lengo hilo.

Alisema kuwa waendelezaji miradi wote walioingia mikataba na REA ya kusambaza umeme katika vijiji 120, hadi sasa ni vijiji 82 kati ya hivyo vimefikiwa na huduma ya umeme na kuagiza vijiji vilivyobaki vikamilishwe ili kutimiza Mpango wa Serikali wa Kusambaza Umeme Vijijini (2016/17 – 2021) la kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote ifikapo Juni 2021.

Mh. Waziri aliwataka waendelezaji hao kujielekeza katika kutimiza lengo hilo la kuvipatia vijiji vyote umeme na kusisitiza ushirikiano wa karibu kati ya sekta binafsi na Serikali kwa ajili ya kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma ya umeme ili kuwawezesha wananchi kujenga uchumi wa viwanda na kuboresha ustawi wa Maisha vijijini. Alisema kuwa hadi sasa kuna jumla ya waendelezaji wa miradi takribani 110 ambapo kati yao, waendelezaji 62 wamepatiwa ruzuku kwa ajili ya kuandaa taarifa za awali lakini ni waendelezaji 18 tu ambao wameanza kujenga na kusambaza miundombinu ya umeme katika maneo mbali mbali yaliyopo nje ya gridi ikiwa ni pamoja na maeneo ya visiwani Tanzania Bara.

Akiongea katika kikao hicho, Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) aliwataka waendelezaji wa miradi ya nishati wawekeze zaidi na kuongeza kiwango cha uzalishaji wa umeme ili utumike katika uanzishwaji wa viwanda.

Awali akimkaribisha Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua alisema lengo la kikao hicho ni kujadili changamoto zinazowakabili waendelezaji wa miradi midogo ya nishati na vilevile kuwafahamisha fursa zilizopo.

Kwa upande wao waendelezaji hao walisema kuwa wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa cheti cha ubora wa mazingira kutoka Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kuomba Serikali kurahisisha upatikanaji wake.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top