Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa
Admin.Frank Mugogo 9403

Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye vijiji na mitaa viliyopo pembezoni mwa miji na majiji. Katika nyakati na maeneo tofauti, uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) pamoja na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) katika maeneo ya Kigamboni, Kisarawe, Mkuranga, Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze.

Akizindua Mradi huo ambao unajulikana kama Peri-urban electrification katika Wilaya ya Kigamboni, Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) alisema Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kuanzisha mradi huu ili kuwasambazia umeme wananchi ambao vijiji au mitaa yao kijiografia inaonekana ipo mijini lakini haijafikiwa na miundombinu kusamba umeme.
Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) ameagiza kifaa cha UMEME TAYARI (UMETA) kifungwe katika nyumba za wananchi ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato cha chini ili nao waweze kunufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Mgalu alitoa agizo hilo wakati akizindua mradi huo katika maeneo ya Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze. Alisema Serikali imetoa UMETA 250 kwa kila LOT ambazo zitatumika kuunganisha umeme kwa wateja ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato kidogo.

Mh. Naibu Waziri alisema wateja wengine watanunua kifaa hicho kwa bei ya Shilingi 36,000 tu na kwamba, wale ambao hawatamudu gharama za kutandaza mfumo wa nyaya za umeme katika nyumba zao wakati wa ujenzi wa miundombinu ya miradi.

Akifafanua kuhusu Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Amos Maganga alisema mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji umeanzishwa kutokana na maombi ya wananchi kupitia wawakilishi wao, ambao waliona nguzo zikipita kwenye miji yao na kupeleka umeme vijijini bila ya wao kunufaika na miundombinu hiyo.

Mhandisi Maganga amesema REA imejipanga kuhakikisha wanavifikia vijiji vyote kwa kufunga transfoma 92 katika maeneo tofauti ya Mkoa wa Pwani ambapo jumla ya shilingi Bilioni 14.9 zitatumika kutekeleza mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«May 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top