Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa
Admin.Frank Mugogo 9496

Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye vijiji na mitaa viliyopo pembezoni mwa miji na majiji. Katika nyakati na maeneo tofauti, uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) pamoja na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) katika maeneo ya Kigamboni, Kisarawe, Mkuranga, Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze.

Akizindua Mradi huo ambao unajulikana kama Peri-urban electrification katika Wilaya ya Kigamboni, Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) alisema Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kuanzisha mradi huu ili kuwasambazia umeme wananchi ambao vijiji au mitaa yao kijiografia inaonekana ipo mijini lakini haijafikiwa na miundombinu kusamba umeme.
Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) ameagiza kifaa cha UMEME TAYARI (UMETA) kifungwe katika nyumba za wananchi ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato cha chini ili nao waweze kunufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Mgalu alitoa agizo hilo wakati akizindua mradi huo katika maeneo ya Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze. Alisema Serikali imetoa UMETA 250 kwa kila LOT ambazo zitatumika kuunganisha umeme kwa wateja ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato kidogo.

Mh. Naibu Waziri alisema wateja wengine watanunua kifaa hicho kwa bei ya Shilingi 36,000 tu na kwamba, wale ambao hawatamudu gharama za kutandaza mfumo wa nyaya za umeme katika nyumba zao wakati wa ujenzi wa miundombinu ya miradi.

Akifafanua kuhusu Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Amos Maganga alisema mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji umeanzishwa kutokana na maombi ya wananchi kupitia wawakilishi wao, ambao waliona nguzo zikipita kwenye miji yao na kupeleka umeme vijijini bila ya wao kunufaika na miundombinu hiyo.

Mhandisi Maganga amesema REA imejipanga kuhakikisha wanavifikia vijiji vyote kwa kufunga transfoma 92 katika maeneo tofauti ya Mkoa wa Pwani ambapo jumla ya shilingi Bilioni 14.9 zitatumika kutekeleza mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top