Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa
Admin.Frank Mugogo 9460

Mradi Mpya wa Kusambaza Umeme Pembezoni mwa Miji na Majiji Wazinduliwa

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye vijiji na mitaa viliyopo pembezoni mwa miji na majiji. Katika nyakati na maeneo tofauti, uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) pamoja na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) katika maeneo ya Kigamboni, Kisarawe, Mkuranga, Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze.

Akizindua Mradi huo ambao unajulikana kama Peri-urban electrification katika Wilaya ya Kigamboni, Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani (Mb) alisema Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kuanzisha mradi huu ili kuwasambazia umeme wananchi ambao vijiji au mitaa yao kijiografia inaonekana ipo mijini lakini haijafikiwa na miundombinu kusamba umeme.
Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu (Mb) ameagiza kifaa cha UMEME TAYARI (UMETA) kifungwe katika nyumba za wananchi ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato cha chini ili nao waweze kunufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Mgalu alitoa agizo hilo wakati akizindua mradi huo katika maeneo ya Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze. Alisema Serikali imetoa UMETA 250 kwa kila LOT ambazo zitatumika kuunganisha umeme kwa wateja ambao ni walemavu, wajane na wenye kipato kidogo.

Mh. Naibu Waziri alisema wateja wengine watanunua kifaa hicho kwa bei ya Shilingi 36,000 tu na kwamba, wale ambao hawatamudu gharama za kutandaza mfumo wa nyaya za umeme katika nyumba zao wakati wa ujenzi wa miundombinu ya miradi.

Akifafanua kuhusu Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Amos Maganga alisema mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji umeanzishwa kutokana na maombi ya wananchi kupitia wawakilishi wao, ambao waliona nguzo zikipita kwenye miji yao na kupeleka umeme vijijini bila ya wao kunufaika na miundombinu hiyo.

Mhandisi Maganga amesema REA imejipanga kuhakikisha wanavifikia vijiji vyote kwa kufunga transfoma 92 katika maeneo tofauti ya Mkoa wa Pwani ambapo jumla ya shilingi Bilioni 14.9 zitatumika kutekeleza mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top