Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini
Aodax K. Nshala 90

Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini

Mitungi 83,500 Yenye Thamani ya Bilioni 3.5 Imetolewa na REA Mpaka Sasa

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali inayo mikakati ya kuhakikisha inaongeza matumizi ya gesi ya kupikia nchini.
 
Ameyasema hayo leo wakati wa mkutano na wananchi wa Mbinga kuhusu nishati safi ya kupikia ambao uliambatana na ugawaji ma mitungi ya gesi Zaidi ya 1500 kwa wananchi wa eneo hilo.
 
“Mpaka sasa kupitia REA tumeshatoa mitungi ya ruzuku 83,500 yenye thamani ya bilioni 3.5 na mwaka huu wa fedha tutatoa mitungi mingine 452,445 yenye thamani ya bilioni 10 ikiwa nia yetu na dhamira yetu ni kupunguza matumizi ya gharama ya kwanza".
 
Aawali akitoa mada kuhusu hatua zilizokwishachukuliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutekeleza maono hayo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anayetaka kufikia 2030 zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, Kaimu Meneja Msaidizi wa Kiufundi REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema Wakala umesambaza zaidi ya majiko banifu 200,000 kwa wananchi.
 
Ameongeza pia Serikali kupitia REA imetenga Shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kuwezesha taasisi zinazohudumia watu Zaidi ya 300 kutumia nishati safi ya kupikia.
 

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«September 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
26
REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Read more
27
Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewaasa wananchi kutunza mazingira na kulinda miundombinu pamoja na vyanzo vya maji ili kuendelea kupata huduma ya umeme pamoja na kuwa na miradi endelevu ya kufua umeme.

Read more
282930311
2345678
9101112
EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

The Government of Tanzania through the Rural Energy Agency (REA) in collaboration with Tanzania Prisons Services (TPS) in response to attainment of sustainable development goals, has opened a   financing   window to support distribution of 15,920 units of 15kg LPG Starter Packs to earmarked Staffs in all Tanzania Prisons. This is part of the Clean Cooking Packages that the parties have agreed to cooperate inorder to enable these institutions to stop using environmentally and healthily harmful cooking solutions.

Read more
131415
16171819202122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top