Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini
Aodax K. Nshala 582

Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini

Mitungi 83,500 Yenye Thamani ya Bilioni 3.5 Imetolewa na REA Mpaka Sasa

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali inayo mikakati ya kuhakikisha inaongeza matumizi ya gesi ya kupikia nchini.
 
Ameyasema hayo leo wakati wa mkutano na wananchi wa Mbinga kuhusu nishati safi ya kupikia ambao uliambatana na ugawaji ma mitungi ya gesi Zaidi ya 1500 kwa wananchi wa eneo hilo.
 
“Mpaka sasa kupitia REA tumeshatoa mitungi ya ruzuku 83,500 yenye thamani ya bilioni 3.5 na mwaka huu wa fedha tutatoa mitungi mingine 452,445 yenye thamani ya bilioni 10 ikiwa nia yetu na dhamira yetu ni kupunguza matumizi ya gharama ya kwanza".
 
Aawali akitoa mada kuhusu hatua zilizokwishachukuliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutekeleza maono hayo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anayetaka kufikia 2030 zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, Kaimu Meneja Msaidizi wa Kiufundi REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema Wakala umesambaza zaidi ya majiko banifu 200,000 kwa wananchi.
 
Ameongeza pia Serikali kupitia REA imetenga Shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kuwezesha taasisi zinazohudumia watu Zaidi ya 300 kutumia nishati safi ya kupikia.
 

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top