Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini
Aodax K. Nshala 140

Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini

Mitungi 83,500 Yenye Thamani ya Bilioni 3.5 Imetolewa na REA Mpaka Sasa

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali inayo mikakati ya kuhakikisha inaongeza matumizi ya gesi ya kupikia nchini.
 
Ameyasema hayo leo wakati wa mkutano na wananchi wa Mbinga kuhusu nishati safi ya kupikia ambao uliambatana na ugawaji ma mitungi ya gesi Zaidi ya 1500 kwa wananchi wa eneo hilo.
 
“Mpaka sasa kupitia REA tumeshatoa mitungi ya ruzuku 83,500 yenye thamani ya bilioni 3.5 na mwaka huu wa fedha tutatoa mitungi mingine 452,445 yenye thamani ya bilioni 10 ikiwa nia yetu na dhamira yetu ni kupunguza matumizi ya gharama ya kwanza".
 
Aawali akitoa mada kuhusu hatua zilizokwishachukuliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutekeleza maono hayo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anayetaka kufikia 2030 zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, Kaimu Meneja Msaidizi wa Kiufundi REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema Wakala umesambaza zaidi ya majiko banifu 200,000 kwa wananchi.
 
Ameongeza pia Serikali kupitia REA imetenga Shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kuwezesha taasisi zinazohudumia watu Zaidi ya 300 kutumia nishati safi ya kupikia.
 

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top