Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Taasisi Zote za Huduma za Kijamii Kuunganishwa na Umeme
Aodax K. Nshala 181

Taasisi Zote za Huduma za Kijamii Kuunganishwa na Umeme

REA Yapongezwa Kufikisha Umeme Katika Shule Vijijini

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema kuwa Taasisi zote zinazotoa huduma za kijamii kama shule na vituo vya afya pamoja na nyumba za ibada zitafikishiwa umeme.

Naibu Waziri Kapinga ameyasema hayo leo Julai 22 wakati akiwasha umeme katika Shule ya Sekondari Nyasa iliyoko katika Kijiji cha Chimate wilayani Nyasa, Mkoa wa Ruvuma. 

“Sisi kama Wizara ya Nishati ni kuhakikisha tunaongeza tija katika taasisi hizi zinazotoa huduma kwa kufikisha umeme. Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan anahangaika usiku na mchana kutafuta fedha za kuboresha maisha ya Watanzania kila siku na kazi yetu kubwa ni kuhakikisha taasisi na maeneo yote yenye umuhumi yanafikiwa na umeme.

Tayari TANESCO na REA wamejidhatiti maeneo ambayo kuna taasisi za kijamii kama shule, vituo vya afya, makanisa, misikiti vyote vinafikiwa na umeme ili kuboresha huduma za kijamii katika Taifa letu,” amesema Naibu Waziri Kapinga.

Amesema kuwa uwepo wa umeme shuleni umesaidia hata kuongeza ufaulu kwa kuwa wanafunzi wamekuwa wakipata muda wa kujisomea hata usiku tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya miradi ya kusambaza umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) haijaanza.

Awali akitoa taarifa, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Eng. Robert Dulle amesema kuwa gharama za kufikisha umeme katika kijiji hicho ni shilingi Milioni 286.

Eng. Dulle ameongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma unajumla ya Vijiji 554 na mpaka kufikia Julai 2024, vijiji 542 sawa na asilimia 97.8 vimepata huduma ya umeme kupitia miradi inayotekelezwa na REA huku akihamasisha wananchin kuchangamkia fursa za uwepo wa umeme vijijini kufanya shughuli za kiuchumi zitakazoboresha maisha yao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Nyasa, Mwalimu John Ndelwa ameipongeza REA kwa kuwafikishia umeme shuleni kwao na kuahidi kuwa watatumia fursa ya kuwepo umeme kuwafundisha wanafunzi masomo ya jioni na hivyo kuongeza ufaulu.

Ameongeza kuwa uwepo wa umeme utawawezesha kuwa na mitihani mingi ya majaribio kwa kuwa watakuwa na uwezo wa kuchapa mitihani wenyewe shuleni tofauti na awali ambapo walikuwa wanalazimika kutumia gharama kubwa kwenda kuchapisha katika steshenari.

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top