Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTAFITI WA HALI YA UPATIKANAJI NA MATUMIZI YA NISHATI YA UMEME TANZANIA BARA KWA MWAKA 2019-2020
Admin.Frank Mugogo 9303

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTAFITI WA HALI YA UPATIKANAJI NA MATUMIZI YA NISHATI YA UMEME TANZANIA BARA KWA MWAKA 2019-2020

Serikali inafanya Utafiti wa Hali ya Upatikanaji na Matumizi ya Umeme Tanzania Bara hususan katika maeneo ya vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (National Bureau of Statistics). Utafiti wa aina hii ni wa pili kufanyika ukihusisha mikoa yote ya Tanzania Bara. Utafiti wa Kwanza ulifanyika kuangalia Hali ya Upatikanaji wa Nishati ya Umeme Tanzania Bara na matokeo yalionesha kuwa upatikanaji wa umeme vijijini na mijini ulikuwa asilimia 49.3 na asilimia 67.5 sawia.

Lengo la utafiti ni kukusanya takwimu rasmi zinazohusu Hali ya Upatikanaji na Matumizi ya Nishati ya Umeme katika ngazi ya kaya na jamii, matumizi ya umeme pamoja na faida zake kwa maendeleo.

Sambamba na ukusanyaji wa takwimu hizi, utafiti huu utahusisha ukusanyaji wa takwimu za kidemografia na za kiuchumi za wanakaya zikijumuisha umri, jinsia, hali ya ndoa, elimu, shughuli za kiuchumi, matumizi ya muda na ushiriki wa jinsia zote katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Utafiti huu utahusisha jumla ya maeneo 1,250, kaya binafsi zipatazo 12,600 pamoja na viongozi wa vijiji na mitaa ambao watahojiwa kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo inayopatikana katika maeneo ya vijijini na mijini yaliyochaguliwa kitaalam katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Utafiti utafanyika kwa mfumo wa kielektroniki ambapo wadadisi watatumia kishikwambi (Tablets) kuwahoji wanakaya na viongozi wa vijiji na mitaa na kisha kujaza majibu ya mahojiano hayo kwenye madodoso. Taarifa zinazokusanywa ni siri na zitatumika kitakwimu tu kwa mujibu wa sheria ya takwimu namba 9 ya mwaka 2015 na marekebisho yake ya mwaka 2019. Taarifa hizo zitatumika kwa madhumuni ya Utafiti huu pekee.

Aidha, taarifa zitakazopatikana zitatumika na Serikali na wadau mbalimbali katika mipango ya maendeleo.

Kutokana na umuhimu wa utafiti huu, natoa wito kwa viongozi wa ngazi zote kuhakikisha wanawahamasisha wananchi wao kutoa ushirikiano kwa wadadisi pindi watakapofika katika maeneo yao. Aidha, nitumie fursa hii kuwaomba Wananchi kutoa ushirikiano kwa wadadisi kwani zoezi hili ni kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu ya Mwaka 2015 na marekebisho yake ya Mwaka 2019.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top