Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTAFITI WA HALI YA UPATIKANAJI NA MATUMIZI YA NISHATI YA UMEME TANZANIA BARA KWA MWAKA 2019-2020
Admin.Frank Mugogo 9269

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTAFITI WA HALI YA UPATIKANAJI NA MATUMIZI YA NISHATI YA UMEME TANZANIA BARA KWA MWAKA 2019-2020

Serikali inafanya Utafiti wa Hali ya Upatikanaji na Matumizi ya Umeme Tanzania Bara hususan katika maeneo ya vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (National Bureau of Statistics). Utafiti wa aina hii ni wa pili kufanyika ukihusisha mikoa yote ya Tanzania Bara. Utafiti wa Kwanza ulifanyika kuangalia Hali ya Upatikanaji wa Nishati ya Umeme Tanzania Bara na matokeo yalionesha kuwa upatikanaji wa umeme vijijini na mijini ulikuwa asilimia 49.3 na asilimia 67.5 sawia.

Lengo la utafiti ni kukusanya takwimu rasmi zinazohusu Hali ya Upatikanaji na Matumizi ya Nishati ya Umeme katika ngazi ya kaya na jamii, matumizi ya umeme pamoja na faida zake kwa maendeleo.

Sambamba na ukusanyaji wa takwimu hizi, utafiti huu utahusisha ukusanyaji wa takwimu za kidemografia na za kiuchumi za wanakaya zikijumuisha umri, jinsia, hali ya ndoa, elimu, shughuli za kiuchumi, matumizi ya muda na ushiriki wa jinsia zote katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Utafiti huu utahusisha jumla ya maeneo 1,250, kaya binafsi zipatazo 12,600 pamoja na viongozi wa vijiji na mitaa ambao watahojiwa kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo inayopatikana katika maeneo ya vijijini na mijini yaliyochaguliwa kitaalam katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Utafiti utafanyika kwa mfumo wa kielektroniki ambapo wadadisi watatumia kishikwambi (Tablets) kuwahoji wanakaya na viongozi wa vijiji na mitaa na kisha kujaza majibu ya mahojiano hayo kwenye madodoso. Taarifa zinazokusanywa ni siri na zitatumika kitakwimu tu kwa mujibu wa sheria ya takwimu namba 9 ya mwaka 2015 na marekebisho yake ya mwaka 2019. Taarifa hizo zitatumika kwa madhumuni ya Utafiti huu pekee.

Aidha, taarifa zitakazopatikana zitatumika na Serikali na wadau mbalimbali katika mipango ya maendeleo.

Kutokana na umuhimu wa utafiti huu, natoa wito kwa viongozi wa ngazi zote kuhakikisha wanawahamasisha wananchi wao kutoa ushirikiano kwa wadadisi pindi watakapofika katika maeneo yao. Aidha, nitumie fursa hii kuwaomba Wananchi kutoa ushirikiano kwa wadadisi kwani zoezi hili ni kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu ya Mwaka 2015 na marekebisho yake ya Mwaka 2019.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top