Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini
Mohamed Saif 10

Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini

Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.

Hayo yamesemwa Julai 15, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu wakati wa hafla ya kuwasha umeme katika Kitongoji cha Mwamlula katika Kijiji cha Mseko na Kitongoji cha Kipeke katika Kijiji cha Masagi Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

“Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo ameuwezesha Wakala wa Nishati Vijijini kuweza kutekeleza majukumu yake kisawasawa na anaendelea kuiwezesha ili kutimiza azma ya kuwafikishia maendeleo wananchi vijijini na vitongojini,” amesema Balozi Kingu.

Amesema mpango uliopo ni kuhakikisha umeme unafika katika vitongoji vyote 64,359 ifikapo Mwaka 2030 na kuwa hadi sasa asilimia 62.4 ya vitongoji tayari vimefikiwa na kwamba hakuna shaka kwa uwezeshwaji unaotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mpango huo utafikiwa kikamilifu.

Amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanatumia umeme kubadilisha maisha yao ya kila siku kama ilivyo azma ya Serikali kwa kuanzisha miradi na shughuli mbalimbali ya kiuchumi kwani umeme ni fursa ya kubadilisha maisha.

“Mnaweza kubadilisha maisha yenu ya kila siku mkaongeza mapato ya kiuchumi kutokana na kufikiwa na umeme kwani pia huduma zingine za kijamii zinazotegemea umeme zitaanzishwa na zingine lkuendelezwa,” amesema.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Thomas Mbaga akizungumza katika hafla hiyo amesema mkoa wa Singida una jumla ya vitongoji 2,289, kati ya hivyo vitongoji 1,196 sawa na 52.25% tayari vimeunganishwa na huduma ya umeme, huku vitongoji 1,093 sawa na 47.75% bado havijafikiwa na huduma hiyo na kwamba utekelezaji wa miradi unaendelea kupitia miradi ya HEP IIA itakayofikisha umeme katika vitongoji 127 na HEP IIB vitongoji 377.

Mha. Mbaga amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanalinda na kutunza miundombinu kwani Serikali inatumia fedha nyingi kutekeleza miradi ya kusambaza umeme na huku akitolea mfano kwa Mkoa wa Singida pekee kuwa hadi sasa takriban shilingi bilioni 94.6 zimetumika kutekeleza miradi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa vitongoji vya Mwamlula na Kipeke wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia umeme na wamebainisha namna ambavyo unakwenda kubadilisha maisha yao.

“Tumefurahi kufikishiwa umeme, ilikuwa ni kama ndoto tu lakini leo hii tumeshuhudia umeme umewashwa na tutajitahidi kuhakikisha tunautumia pia kujiongezea kipato mbali na kutuangazia wakati wa usiku,” amesema Lucia Constantine mkazi wa kitongoji cha Mwamlula.

 

Share

Print
«July 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
131415
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini

Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini

Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.

Read more
16171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top