Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 8308

TAARIFA KWA WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI ZA KUTEKELEZA MRADI KABAMBE WA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umekamilisha taratibu za zabuni kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (Turnkey III). Mradi huu unahusisha kupeleka umeme wa gridi kwenye Vijiji 3559 katika Mikoa 25 ya Tanzania Bara. Hatua zinazofuata ni Wakandarasi walioshinda kupewa barua za tuzo (Award Letters) na kusaini mikataba kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa Mradi.

Utoaji wa barua hizi unafuatia kukamilika kwa mchakato wa kuwapata wazabuni watakaotekeleza mradi huo uliogawanywa katika mafungu (Lots) 29. Wazabuni wanaopewa barua wanatakiwa kukamilisha vigezo na masharti yaliyotajwa katika barua za tuzo kabla ya kusaini mikataba ya utekelezaji wa Mradi.

Aidha, Wakala umeandaa Mkutano maalum kwa Wakandarasi kwa ajili ya kuwakabidhi barua za tuzo (Award Letters). Mkutano huo utafanyika tarehe 18 Mei 2017 kuanzia saa 8 mchana katika Ukumbi wa Hazina uliopo katika Manispaa ya Dodoma.

Wazabuni wote walioshinda wanatakiwa kushiriki katika Mkutano huu.

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Sam Nujoma, 14414
S. L. P 7990
Dar es Salaam.
Simu +255 22 2412001/2/3

Barua pepe: info@rea.go.tz

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top