Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 8285

TAARIFA KWA WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI ZA KUTEKELEZA MRADI KABAMBE WA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umekamilisha taratibu za zabuni kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (Turnkey III). Mradi huu unahusisha kupeleka umeme wa gridi kwenye Vijiji 3559 katika Mikoa 25 ya Tanzania Bara. Hatua zinazofuata ni Wakandarasi walioshinda kupewa barua za tuzo (Award Letters) na kusaini mikataba kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa Mradi.

Utoaji wa barua hizi unafuatia kukamilika kwa mchakato wa kuwapata wazabuni watakaotekeleza mradi huo uliogawanywa katika mafungu (Lots) 29. Wazabuni wanaopewa barua wanatakiwa kukamilisha vigezo na masharti yaliyotajwa katika barua za tuzo kabla ya kusaini mikataba ya utekelezaji wa Mradi.

Aidha, Wakala umeandaa Mkutano maalum kwa Wakandarasi kwa ajili ya kuwakabidhi barua za tuzo (Award Letters). Mkutano huo utafanyika tarehe 18 Mei 2017 kuanzia saa 8 mchana katika Ukumbi wa Hazina uliopo katika Manispaa ya Dodoma.

Wazabuni wote walioshinda wanatakiwa kushiriki katika Mkutano huu.

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Sam Nujoma, 14414
S. L. P 7990
Dar es Salaam.
Simu +255 22 2412001/2/3

Barua pepe: info@rea.go.tz

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top