Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 8638

TAARIFA KWA WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI ZA KUTEKELEZA MRADI KABAMBE WA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umekamilisha taratibu za zabuni kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (Turnkey III). Mradi huu unahusisha kupeleka umeme wa gridi kwenye Vijiji 3559 katika Mikoa 25 ya Tanzania Bara. Hatua zinazofuata ni Wakandarasi walioshinda kupewa barua za tuzo (Award Letters) na kusaini mikataba kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa Mradi.

Utoaji wa barua hizi unafuatia kukamilika kwa mchakato wa kuwapata wazabuni watakaotekeleza mradi huo uliogawanywa katika mafungu (Lots) 29. Wazabuni wanaopewa barua wanatakiwa kukamilisha vigezo na masharti yaliyotajwa katika barua za tuzo kabla ya kusaini mikataba ya utekelezaji wa Mradi.

Aidha, Wakala umeandaa Mkutano maalum kwa Wakandarasi kwa ajili ya kuwakabidhi barua za tuzo (Award Letters). Mkutano huo utafanyika tarehe 18 Mei 2017 kuanzia saa 8 mchana katika Ukumbi wa Hazina uliopo katika Manispaa ya Dodoma.

Wazabuni wote walioshinda wanatakiwa kushiriki katika Mkutano huu.

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Sam Nujoma, 14414
S. L. P 7990
Dar es Salaam.
Simu +255 22 2412001/2/3

Barua pepe: info@rea.go.tz

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
4567
891011121314
15161718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top