Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 20679

UTEKELEZAJI WA MRADI KABAMBE WA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU (TURNKEY III) WAANZA

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imeanza utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Awamu ya Tatu wa kusambaza nishati vijijini utakaojumuisha vijiji 7,873 katika wilaya na mikoa yote ya Tanzania Bara ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia mwaka huu wa fedha 2016/17 hadi 2020/21. Kati ya vijiji hivyo, vijiji 7,697 vitapelekewa umeme wa gridi na vijiji 176 umeme wa nje ya gridi (off-grid).

Utekelezaji wa Mradi huu unajumuisha vipengele-mradi (project components) vitatu:

1. Densification - kuongeza wigo wa miundombinu ya usambazaji umeme (underline distribution trasformers) katika maeneo yenye miundombinu ili kufikisha umeme kwenye vitongoji ambavyo havijafikiwa na umeme;

2. Grid extension - kinacholenga kufikisha umeme kwenye vijiji ambavyo havijafikiwa kabisa na miundombinu ya umeme wa gridi; na

3. Off-grid Renewable - Uzalishaji na usambazaji wa nishati jadidifu kwenye maeneo yaliyo mbali na miundombinu ya umeme wa gridi (off-grid) na kwenye visiwa.

Utekelezaji wa vipengele-mradi katika Mradi huu umeanza na upo katika hatua mbalimbali kama ilivyoainishwa hapa chini.

Kipengele-mradi cha Densification

Utekelezaji wake tayari umeanza kufuatia Mikataba iliyosainiwa Mwezi Desemba, 2016 katika mikoa sita ya Arusha, Iringa, Mara, Mbeya, Pwani, na Tanga kwa gharama ya Dola za Marekani Milioni 27 kutoka Serikali ya Tanzania na Norway, hivyo kuwezesha vijiji 305 kusambaziwa umeme.

Kipengele-mradi cha Grid Extension

• Kusambaza umeme kwenye vijiji 3,559 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara unaokadiriwa kugharimu Shilingi bilioni 733.98 kutoka Serikali ya Tanzania, Norway, Sweden na Benki ya Dunia. Mradi utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 24 kuanzia mwaka wa fedha 2016/17 hadi 2017/18. Taratibu za ununuzi zinaendelea na wakandarasi wataanza kazi mwezi Machi 2017. Hadi sasa jumla ya vijiji 4,395 kati ya vijiji 12,268 ambayo ni sawa asilimia 36 vimeunganishwa na huduma ya umeme. Baada ya kukamilika kwa mradi huu, jumla ya vijiji 7,934 sawa na asilimia 65 vitakuwa vimefikiwa na umeme. Vijiji 4,334 vinavyosalia vitapelekewa umeme kuanzia mwaka wa fedha 2018/19 hadi 2020/21 kutegemeana na upatikanaji wa fedha.

• Kusambaza umeme kwenye vijiji 121 katika maeneo yanayopitiwa na umeme wa Msongo wa Kilovoti 400 kutoka katika mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida, Tabora na Shinyanga kwa gharama ya dola za Marekani milioni 30 kwa ufadhili wa Serikali za Norway na Sweden. Taratibu za ununuzi wa wakandarasi zinakamilishwa na utekelezaji utaanza mwezi Machi 2017.

Kipengele-Miradi cha Umeme wa Nje ya Gridi (Off-grid Renewable)

Miradi hii inayotekelezwa na sekta binafsi inahusisha kuendeleza na kusambaza nishati jadidifu kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi pamoja na kwenye Visiwa vilivyopo kwenye maziwa na katika Bahari ya Hindi. Jumla ya Dola za Marekani milioni 84 zimetengwa kwa ajili ya mradi huu ; kati ya hizo Dola za Marekani milioni 42 ni kutoka Serikali ya Uingereza na Dola za Marekani milioni 42 kutoka Benki ya Dunia. Wakala ulitangaza awamu ya kwanza ya mradi huu tarehe 23 Septemba, 2016 (1st Call for Proposals) kwa ajili ya kushindanisha waendelezaji binafsi na wajasiriamali wa nishati jadidifu kwenye maeneo ya nje ya gridi (off-grid mini grids). Awamu ya pili itatangazwa mwezi Aprili 2017, matangazo haya yatakuwa yanatolewa kwa awamu kila baada miezi sita. Wajasiriamali wa nishati jadidifu wanahamasishwa kushiriki katika utekelezaji wa mradi huu.

Hitimisho

Wakala unaishukuru Serikali kwa kuweka msisitizo kwenye miradi ya usambazaji wa nishati bora vijijini pamoja na kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo. Lengo la Serikali ni kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania Bara ifikapo Mwaka 2021; na kuongeza idadi ya vijiji vilivyofikiwa na huduma ya umeme hadi asilimia 85 mwaka 2025 na asilimia 100 Mwaka 2030.


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print

Documents to download

«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top