Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Uzinduzi wa Tovuti ya Miradi Midogo ya Umeme (Minigrids Portal)
Aodax K. Nshala 5879

Uzinduzi wa Tovuti ya Miradi Midogo ya Umeme (Minigrids Portal)

Event date: 8/11/2016 Export event

Kwa Ushirikiano na Benki ya Dunia Kupitia International Finance Corporation (IFC)

Serikali ya Jamhuri ya Muugano wa Tanzania imezindua tovuti inayotoa taarifa za fursa na taratibu za uwekezaji kwenye miradi midogo ya umeme nje ya gridi ya Taifa.

Uzinduzi wa tovuti hiyo ulifanyika tarehe 11 Agosti, 2016 katika Ofisi za Benki ya Dunia Tanzania. Lengo la tovuti hiyo ni kutoa taarifa ambazo zitawawezesha waendelezaji wa miradi ya nishati bora vijijini, wawekezaji mbalimbali pamoja na wadau wengine kupata taarifa sahihi ambazo zitachangia katika kuongeza wigo wa usambazaji na upatikanaji wa nishati bora vijijini.

Tovuti hiyo inatoa taarifa za kina kwa waendelezaji na wawekezaji kwenye miradi midogo ya nishati jadidifu nchini Tanzania.

Uanzishwaji wa tovuti hii umefanyika chini ya mradi wa SREP (Scaling-Up Renewable Energy Program) ambao unachochea uwekezaji kwenye nishati jadidifu ikijumuisha miradi midogo ya umeme (minigrids).

Tovuti hiyo, www.minigrids.go.tz inasimamiwa na kuhifadhiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na taarifa zake zinaratibiwa kwa ushirikiano wa uwakilishi wa wadau wengine ambao ni Wizara ya Nishati na Madini (MEM), EWURA, NEMC, TAREA, TBS pamoja na TANESCO.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«January 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2930311234
5678910
Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kata za Wendele na Mwendakulima Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadilisha maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
11
12131415161718
19202122232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top