Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi
Mohamed Saif 880

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Wabunge waimwagia sifa REA

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema hayo Aprili 22, 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati anawasilisha taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 katika Bunge la 13 Mkutano wa Tatu, Kikao cha Kumi na Nne.

“Mwelekeo wa Serikali ni kuhakikisha umeme unafikishwa katika vitongoji vyote Tanzania Bara na ili kufikia azma hiyo, Serikali ilianza utekelezaji wa mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika Vitongoji 9,009 ambao utakamilika katika kipindi cha miaka mitatu ijayo,” amesema Waziri Ndejembi.

Amefafanua kuwa miradi inayoendelea kutekelezwa ya kupeleka umeme vitongojini itawezesha vitongoji 50,453 sawa na asilimia 78.4 ya vitongoji vyote vya Tanzania Bara kufikishiwa huduma ya umeme ifikapo mwaka 2028, hatua ambayo itachochea kasi ya ukuaji wa uchumi vitongojini.

Waziri Ndejembi ametaja hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali katika kupeleka nishati vijijini ni kuwa ni pamoja na kuanza utekelezaji wa mradi wa kuongeza uunganishaji wa wateja katika vitongoji (Universal Hamlet Eletrification and Last Mile Customers Connectivity) katika mikoa ya Pwani, Morogoro na Dodoma ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mahsusi wa Nishati wa Taifa (National Energy Compact) ulioridhiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika (Mission 300) mwezi Januari, 2025.

Hatua nyingine ni utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 3,060 sawa na vitongoji 15 kwa kila Jimbo ambao amesema umefikia 80% ya utekelezaji.

“Serikali iliendelea na utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme katika Vitongoji vya Mikoa ya Songwe, Kigoma na Lindi pamoja na maeneo ya migodi midogo ikiwemo iliyopo Chunya (Mbeya) na Kwa Msisi Handeni (Tanga) na viwanda na kilimo katika Mikoa ya Ruvuma, Njombe, Mbeya na Rukwa ili kuchochea shughuli za kiuchumi katika mikoa hiyo, ambapo utekelezaji upo hatua mbalimbali,” amebainisha Waziri Ndejembi.

Katika kuhakikisha kuwa maeneo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa yanafikiwa na huduma za umeme Waziri Ndejembi amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) iliendelea na utekelezaji wa mradi wa kusambaza mifumo ya jua inayojitegemea (Solar Home System-SHS) katika makazi 20,000 katika visiwa vidogo 143 vilivyopo katika Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika ambapo hadi Machi, 2026 jumla ya makazi 1,302 yalikuwa yamefungiwa mifumo hiyo. 

Aidha, akizungumzia eneo la Nishati Safi ya Kupikia, Waziri Ndejembi amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, inaendelea na utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024 - 2034) uliozinduliwa mwezi Mei, 2024, wenye lengo la kuhakikisha angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

“Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kiafya na kimazingira na kuwezesha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi na katika taasisi hususan, zinazohudumia watu zaidi ya 100,” amefafanua Waziri Ndejembi.

Amesema kuwa kutokana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali, matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini yameendelea kuimarika kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 28.6 ya watanzania wenye nishati safi ya kupikia mwaka 2025, hatua ambayo amesema inachangia katika kupunguza uharibifu wa mazingira dhidi ya matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia na pia kulinda afya za wananchi dhidi ya matumizi ya nishati zisizo safi za kupikia.

“Kwa namna ya kipekee, nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongea Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa maono na uongozi wake uliotuwezesha kuwa na mwelekeo huu wa kitaifa wa kuhakikisha wananchi wetu wanatumia nishati safi ya kupikia, ajenda ambayo imempa heshima ya kuwa kinara wa nishati safi ya kupikia Barani Afrika na kimataifa,” amesema Waziri Ndejembi.

Kwa nyakati tofauti wakichangia katika hotuba hiyo ya Nishati, wabunge waliipongeza REA kwa hatua iliyofikia ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme na miradi ya nishati safi ya kupikia sambamba na

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top