Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Mmebeba Ajenda Ya Rais Samia- Subira Mgalu
Mohamed Saif 110

REA Mmebeba Ajenda Ya Rais Samia- Subira Mgalu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inaridhishwa na namna ambavyo Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza miradi ya Kusambaza Nishati Vijijini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu amesema hayo Aprili 22, 2026 alipotembelea Banda la REA kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

"REA mmeibeba vyema ajenda ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Nishati Safi ya Kupikia inawafikia wananchi wengi wa Vijijini," amesema Mhe. Mgalu

Amesisitiza uhamasishaji na Elimu ya Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iendelee kutolewa ili kufanikisha lengo la Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Amesema Kamati anayoiongoza pamoja na Wabunge wataendelea kuwa mabalozi wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwani tayari wanao uelewa wa kutosha.

Aidha, kuhusu suala la usambazaji wa umeme, Mhe. Mgalu amesema kazi kubwa imetekelezwa na REA kwani tayari vijiji vyote nchini vimefikishiwa umeme na kwamba Miradi inaendelea kutekelezwa ya kufikisha vitongojini.

Kwa nyakati tofauti, Wabunge waliotembelea Banda la REA walieleza kuridhishwa kwao na hatua za utekelezaji wa miradi zinazoendelea kuchukuliwa na REA.

 

Share

Print
«July 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
131415
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini

Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wananchi Vitongojini

Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.

Read more
16171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top