Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali Kutekeleza Miradi ya REA Kusambaza Nishati Vijijini
Admin.Frank Mugogo 686

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali Kutekeleza Miradi ya REA Kusambaza Nishati Vijijini

Zaidi ya Shilingi Trilioni 4 zimetolewa hadi sasa

Serikali na Wabia wa Maendeleo Katika Sekta ya Nishati (EDPG) wamechangia zaidi ya shilingi trilioni nne kwa ajili ya Miradi ya kusambaza nishati vijijini inayotekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila amesema kuwa toka REA ianzishwe, Serikali imechangia jumla ya Shilingi Trilioni tatu wakati Wabia wa Maendeleo wamechangia Shilingi Trilioni moja kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini (REF).

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka kati ya REA na Wabia wa Maendeleo wanaofadhili Miradi ya kusambaza nishati vijijini uliofanyika tarehe 27 Mei 2022 katika hoteli ya Salinero iliyopo mkoani Kilimanjaro, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Rwebangila alisema kuwa fedha hizo zimetumika kupeleka miundombinu ya umeme katika ngazi ya vijiji. “Hatua ya kwanza ni kupeleka miundombinu ya umeme katika vijiji vyote na ifikapo Desemba mwaka huu tuwe tumegusa kila kijiji. Hii ilikuwa ni hatua ya kupeleka umeme katika vijiji na watu wengi wanalalamika kuwa hawajafikiwa na huduma ya umeme. Hawa wadau wa maendeleo wakati Serikali ikipeleka miundombinu wamekuwa wakitusaidia kujazia yale maeneo ambayo yameshafikiwa na miundombinu” alisema.

Mhandisi Rwebangila alisema kuwa kulinga na kiwango cha fedha za bajeti ambacho kinatolewa kila mwaka itachukua miaka kati ya 18 hadi 20 kukamilisha kupeleka umeme katika vitongoji vyote. Hivyo Wizara inapanga mikakati ambayo itapunguza huo muda wa kupeleka umeme katika vitongoji ufikie miaka mitano. “Tunafurahi kuwa tunapata changamoto kwa maendeleo tuliyoleta, wakati tunaanza wachache sana walihamasika na umeme, lakini leo kila mtu amehamasika.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy alisema kuwa, lengo la Mkutano huo ni kujadili Mpango Kazi wa Mwaka Pamoja na bajeti ya Wakala. “Tunatambua mchango wa Wabia wa Maendeleo ambao wanatoa fedha za kutekeleza Miradi ya kusambaza nishati vijijini kwa lengo la kuwapatia wananchi nishati bora. Nawashukuru na kuwapongeza Wabia wetu kwa msaada ambao wamekuwa wakitoa toka kuanzishwa kwa Wakala”.

Mhandisi Saidy alisema kuwa jitihada za Serikali na Wabia wa Maendeleo zimewezesha upatikanaji wa huduma za umeme vijijini kuongezeka kutoka asilimia mbili Mwaka 2007 wakati Wakala unaanzishwa hadi kufikia asilimia 70 Mwaka 2020.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amewashukuru Wabia wa Maendeleo kwa mchango wao katika Miradi ya kusambaza nishati vijijini. “Nitumie fursa hii kuwashukuru Wabia wa Maendeleo kwa sababu wamekuwa wakichangia mpaka asilimia 25 ya bajeti ya Wakala wa Nishati Vijijini kwa ajili ya Miradi ya kusambaza nishati vijijini. Mkutano huu kwa kawaida unatusaidia kuwapeleka Wabia wa Maendeleo katika Miradi waliyofadhili kuweza kuona utekelezaji wa Miradi na tija ya Miradi hiyo kwa wananchi”, alisema.

Awali akifungua Mkutno huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Steven Kigaigai aliipongeza REA kwa kazi kubwa ambayo wameifanya ya kusambaza miundombinu ya umeme vijijini. “Katika Mkoa wa Kilimanjaro, vijiji 11 tu ndiyo havina umeme, hivyo nawapongeza na kuwashukuru. Bado tunawahitaji REA kwa sababu ya mahitaji makubwa ya kuleta maendeleo ya nchi”, alisema.

Mwenyekiti wa EDPG, Bjorn Midthun aliipongeza REA na Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri ya kusambaza nishati vijijini ambayo aliitaja kuwa inalenga kutimiza malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yenye azma ya kuondoa umaskini na kuna umuhimu wa watu wa vijijini kupata umeme wa bei nafuu ili waweze kuutumia katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na huduma za elimu, afya, maji pamoja na kutunza mazingira kwa ajili ya kuboresha ustawi wa maisha ya watu vijijini.

Midthun alisema Wabia wa Maendeleo wameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini na kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi hiyo. Hata hivyo, alishauri REA kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania wafanye tathimini ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini kwa ajili ya kujua mafanikio na changamoto za utekelezaji wake na kuweka mikakati ya baadaye.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top