Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA
Frank A. Mugogo 13

Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa waendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu kote nchini kuchangamkia fursa za uwezeshwaji zinazotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kuwa na miradi yenye tija kwa Taifa.

Ametoa wito huo Juni 19, 2025 akiwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua mradi wa kuzalisha umeme wa Mwenga wa megawati nne unaomilikiwa na Kampuni ya Mwenga Hydro Limited kwa kutumia maporomoko ya Mto Mwenga katika Kijiji cha Ifwagi, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

"Kwenye eneo hili la nishati jadidifu fursa zilizopo ni nyingi, Tanzania ni kubwa na imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi na bado hazijatumika ipasavyo; tunahitaji waendelezaji wengi wa miradi ya kuzalisha umeme kwa upepo, joto ardhi, jua na maporomoko ya maji kujitokeza ili kuwezeshwa na REA kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa umeme nchini," alisema Mhe. Balozi Kingu.

Alisisitiza kuwa waendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu ni muhimu katika kuharakisha maendeleo ya Taifa hasa ikizingatiwa kuwa umeme ni miongoni mwa nyenzo muhimu katika kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Taifa.

Alisema tangu REA imeanza kuwezesha waendelezaji wa miradi hiyo ya nishati jadidifu mchango wao umeonekana kuanzia ngazi ya chini ya eneo la mradi ambao umenufaisha vijiji vinavyozunguka hadi ngazi ya Taifa kupitia umeme wanaoingiza katika Gridi ya Taifa.

"Waendelezaji wadogo wa miradi hii ni muhimu kwani mchango wao kwa Taifa unaonekana; sisi tunaahidi kuendelea kuwaunga mkono kwa kuwawezesha kwa namna mbalimbali ikiwemo ruzuku pamoja na mikopo nafuu ya muda mrefu sambamba na kuwajengea uwezo wa kitaalamu," alifafanua Mhe. Balozi Kingu.

Akizungumzia mradi huo wa Mwenga, Mhe. Balozi Kingu alisema Bodi anayoiongoza inajivunia mchango wa REA katika mradi na alitoa wito kwa uongozi wa mradi kuwasilisha andiko la kuongeza Kasi ya upatikanaji wa umeme nchini.

"Nimeelezwa mmepata chanzo kingine cha kuzalisha umeme ambacho kinaweza kutupatia takriban megawati 10, fanyeni hima kuwasilisha andiko lake ili nasi tuanze taratibu stahiki; tunahitaji mirdi mingi ya namna hii ili kuliongezea nguvu Shirika la Umeme (TANESCO)," alisema.

Akiwasilisha taarifa ya Mradi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Rift Valley Energy kampuni mama ya Mwenga Hydro Limited, Michael Gratwicke aliishukuru REA kwa uwezeshwaji mkubwa iliyofanya katika mradi huo.

"Tunaishukuru REA kwani leo hii tunahudumia takriban kaya 10,000 ndani ya vijiji 32 kutokana na uwezeshwaji wa REA; tusingefika hapa kama isingekuwa uwezeshwaji huu," alisema Gratwicke.

Akizungumza kuhusiana na uwezeshwaji kwa ujumla, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alisema REA ilitoa ruzuku ya takriban shilingi bilioni 23 kuendeleza mradi huo.

"Serikali kupitia REA imewezesha mradi huu kwa kutoa kiasi cha fedha takribani shilingi bilioni 23 ikiwemo shilingi bilioni 18 ya kuwaunganisha wateja na shilingi bilioni 5 ambayo ilitolewa Kama mkopo wa mda mrefu ili kuwezesha ujenzi wa Mradi huo," alifafanua Mha. Mwijage.

Alisema kuwa Wakala unatoa kipaumbele kwenye ujenzi wa miradi ya nishati jadidifu nchini ili kusaidia utunzaji wa mazingira, kuboresha upatikanaji wa umeme, kuongeza uzalishaji wa umeme unaotokana na nishati Jadidifu pamoja na kutoa ajira kupitia miradi hiyo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«June 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Read more
28
Lesotho Wavutiwa na REA

Lesotho Wavutiwa na REA

Serikali ya Lesotho imevutiwa na namna ambavyo Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijiji (REA) imepiga hatua katika suala zima la usambazaji wa nishati safi maeneo ya vijijini.

Read more
293031
REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala

REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala

Wakala wa Nishati Vijijini unahamasisha wananchi kote nchini kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo Mkaa mbadala ambao umeelezwa kuwa na gharama nafuu na ni salama kwa afya ya mtumiaji na mazingira.

Read more
1
23
The National Clean Cooking Communication Strategy launched

The National Clean Cooking Communication Strategy launched

Tanzania is embarking on a bold and transformative journey that places clean cooking at the heart of public health, environmental protection, and inclusive development. Global data shows that over 2.1 billion people lack access to clean cooking solutions. In Sub-Saharan Africa, nearly one billion people remain reliant on polluting fuels, and Tanzania stands among the countries most in need of an accelerated transition.

Read more
45678
9101112131415
161718
Waendelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Lupali Mkoani Njombe Waelekezwa Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Mradi

Waendelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Lupali Mkoani Njombe Waelekezwa Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Mradi

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu ameelekeza waendelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme wa kilowati 317 kwa kutumia maporomoko ya Mto Lupali kuimarisha ulinzi na usalama wa mradi ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

Read more
1920
Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA

Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa waendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu kote nchini kuchangamkia fursa za uwezeshwaji zinazotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kuwa na miradi yenye tija kwa Taifa.

Read more
2122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top