Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam
Frank A. Mugogo 66

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Hafla ya ugawaji wa mitungi na majiko yake iliongozwa na Mhe. Balozi, Radhia Msuya, Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vjijini (REB) katika gereza la ukonga, Jijini, Dar es Salaam, leo Juni 30, 2025 ambapo kwa upande wa Magereza uliwakilishwa na Msaidizi wa Mkuu wa Gereza hilo, Kamishna Msaidizi, (ACP); Athuman Recha.

Balozi, Radhia amesema kuwa, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Watumishi hao watasambaziwa mitungi ya gesi na majiko yapatayo 464 na kuongeza kuwa huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Awamu ya Sita; Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kama nyenzo ya kulinda afya za Watanzania, kulinda na kutunza mazingira 

Amesema kuwa, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeingia makubaliano na Jeshi la Magereza ili kuwawezesha, kuhama kutoka katika matumizi ya nishati isiyo salama kwenda katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika magereza yote nchini. 

“Serikali kupitia REA, ilishaanza uwezeshaji kwa Jeshi la Magereza na wameshaanza kutumia Nishati Safi na kwa msisitizo huo, tuliona ni vyema, kuwawezesha Watumishi na Maafisa ili nao waachane na nishati chafu ili kulinda afya zao pamoja na kulinda mazingira yetu”. Amesema, Mhe. Balozi, Radhia.

Naye, Mkurugenzi wa Fedha na Uwezeshaji, CPA, Daniel Mungure ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), amewataka watumishi wa jeshi la magereza  kuibeba Ajenda ya Mhe. Rais Samia ya kuwa Mabalozi wa Nishati Safi ya kupikia kwa kuendelea kutumia gesi na siyo kuni na mkaa.

Akishukuru kwa uwezeshaji huo kwa Watumishi na Maafisa wa Jeshi la Magereza, Mrakibu Mwandamizi, (SSP); Moses Mumbi amesema, wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwajali na kuongeza kuwa teknolojia hizo za Nishati Safi ya Kupikia si tu zinalinda afya zao lakini zinaongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao wakati wa kuwahudumia Mahabusu na Wafungwa.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top