Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
WATEJA 22,700 KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME KUTOKA MAKAMBAKO HADI SONGEA
Admin.Frank Mugogo 10930

WATEJA 22,700 KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME KUTOKA MAKAMBAKO HADI SONGEA

WATEJA 22,700 KUNUFAIKA NA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME KATIKA VIJIJI VINAVYOPITIWA NA MKUZA WA MRADI WA UMEME KUTOKA MAKAMBAKO HADI SONGEA

Jumla ya wateja wa awali 22,700 wanatarajiwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia Mradi wa Kusambaza Umeme katika mkuza wa njia kuu ya kusafirisha umeme wa kilovolti 220 kutoka Makambako hadi Songea. Mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Ruvuma na Njombe ambapo jumla ya vijiji 122 vinatarajiwa kupelekewa miundombinu ya kusambaza umeme na tayari vijiji 110 vimefikishiwa huduma ya umeme.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi huo tarehe 06/04/2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli aliwataka wananchi wanaoishi katika vijiji vilivyopo katika mradi huo kutumia umeme kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo na kuleta maendeleo. Aidha, Rais aliagiza vijiji vyote ambavyo havina umeme visambaziwe miundombinu na kuwezesha upatikanaji wa huduma ya umeme katika vijiji hivyo.

Awali Bodi ya Nishati Vijijini (REB) iliwahakikishia wananchi waishio maeneo ya vijijini nchini kuwa watapelekewa huduma ya umeme kupitia Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ambao utakamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme katika vijiji vyote ambavyo bado havijafikiwa na miundombinu ya umeme.
Naye Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Anders Sjöberg ambaye nchi yake imefadhili mradi huo alisema anaamini kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha utoaji wa huduma za afya, elimu, maji pamoja na kuongeza kipato hivyo kupunguza umaskini.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«May 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top