Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 7792

BALOZI WA NORWAY ATEMBELEA OFISI ZA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA)

Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ms. Elisabeth Jacobsen ametembelea Ofisi za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Wakala tarehe 28 Februari, 2019.
Katika mazungumzo hayo, Mh. Balozi alisema ziara yake hiyo ina lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Wakala na Ubalozi ikizingatiwa kuwa sekta ya nishati ni moja ya maeneo ya kipaumbele kwa nchi ya Norway katika ushirikiano. Aliongeza kuwa, sekta ya nishati imevutia wawekezaji na imesaidia kukuza sekta binafsi.

Awali Balozi Jacobsen na ujumbe wake walitembelea wajasiriamali katika Wilaya ya Mkuranga ambao wamenufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Balozi alisema wamevutiwa na shughuli za uzalishaji mali ambazo zimeibuka katika maeneo ya vijijiini kutokana na upatikanaji wa huduma za umeme hivyo kuwawezesha wananchi kuongeza kipato na kubadilisha hali za maisha yao.

Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini ilishukuru na kusisitiza ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ili kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Awali akiwakaribisha wageni hao, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Amos Maganga aliishukuru Serikali ya Norway kwa kufadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini na kuwaomba waendelee kutoa ufadhili kwa Serikali ili iweze kusambaza nishati katika maeneo ya visiwa zaidi ya 100 vilivyopo katika maziwa mbalimbali na Bahari ya Hindi.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
1718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top