Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 7537

BALOZI WA NORWAY ATEMBELEA OFISI ZA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA)

Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ms. Elisabeth Jacobsen ametembelea Ofisi za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Wakala tarehe 28 Februari, 2019.
Katika mazungumzo hayo, Mh. Balozi alisema ziara yake hiyo ina lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Wakala na Ubalozi ikizingatiwa kuwa sekta ya nishati ni moja ya maeneo ya kipaumbele kwa nchi ya Norway katika ushirikiano. Aliongeza kuwa, sekta ya nishati imevutia wawekezaji na imesaidia kukuza sekta binafsi.

Awali Balozi Jacobsen na ujumbe wake walitembelea wajasiriamali katika Wilaya ya Mkuranga ambao wamenufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Balozi alisema wamevutiwa na shughuli za uzalishaji mali ambazo zimeibuka katika maeneo ya vijijiini kutokana na upatikanaji wa huduma za umeme hivyo kuwawezesha wananchi kuongeza kipato na kubadilisha hali za maisha yao.

Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini ilishukuru na kusisitiza ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ili kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Awali akiwakaribisha wageni hao, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Amos Maganga aliishukuru Serikali ya Norway kwa kufadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini na kuwaomba waendelee kutoa ufadhili kwa Serikali ili iweze kusambaza nishati katika maeneo ya visiwa zaidi ya 100 vilivyopo katika maziwa mbalimbali na Bahari ya Hindi.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top