Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 7490

BALOZI WA NORWAY ATEMBELEA OFISI ZA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA)

Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ms. Elisabeth Jacobsen ametembelea Ofisi za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Wakala tarehe 28 Februari, 2019.
Katika mazungumzo hayo, Mh. Balozi alisema ziara yake hiyo ina lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Wakala na Ubalozi ikizingatiwa kuwa sekta ya nishati ni moja ya maeneo ya kipaumbele kwa nchi ya Norway katika ushirikiano. Aliongeza kuwa, sekta ya nishati imevutia wawekezaji na imesaidia kukuza sekta binafsi.

Awali Balozi Jacobsen na ujumbe wake walitembelea wajasiriamali katika Wilaya ya Mkuranga ambao wamenufaika na miradi ya kusambaza umeme vijijini. Mh. Balozi alisema wamevutiwa na shughuli za uzalishaji mali ambazo zimeibuka katika maeneo ya vijijiini kutokana na upatikanaji wa huduma za umeme hivyo kuwawezesha wananchi kuongeza kipato na kubadilisha hali za maisha yao.

Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini ilishukuru na kusisitiza ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ili kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Awali akiwakaribisha wageni hao, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Amos Maganga aliishukuru Serikali ya Norway kwa kufadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini na kuwaomba waendelee kutoa ufadhili kwa Serikali ili iweze kusambaza nishati katika maeneo ya visiwa zaidi ya 100 vilivyopo katika maziwa mbalimbali na Bahari ya Hindi.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top