Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri wa Nishati Zanzibar Aipa Kongole REA
Frank A. Mugogo 147

Waziri wa Nishati Zanzibar Aipa Kongole REA

Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe. Shaib Kaduara ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhakikisha huduma za Nishati zinafika katika maeneo yote ya Vijiji Tanzania Bara.

Ametoa pongezi hizo Jijini Dar es Salaam Oktoba 25, 2024 alipotembelea Banda la Wakala kabla ya kufunga Kongamano la 10 la Jotoardhi (ARGeo-C10).

Mhe. Kaduara aliisisitiza REA kuhakikisha inaongeza nguvu katika suala la uhamasishaji ili kuwezesha wananchi umuhimu wa kubadilika na kuachana na matumizi ya nishati ambazo sio safi na salama kwa afya zao na kwa mazingira.

"Hongereni mnafanya kazi nzuri, muhimu ni kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi waelewe umuhimu wa kubadilika na kuachana na matumizi ya Nishati chafu," alielekeza.

Awali akitoa maelezo ya majukumu ya REA, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage alisema Wakala unatekeleza Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) ambao ulizinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhandisi Mwijage amesema REA inatekeleza program mbalimbali ili kuhakikisha wananchi hususan wa maeneo ya vijijini wanapunguza na baadae kuachana kabisa na matumizi ya nishati chafu za kupikia ikiwemo kuni na mkaa.

"Tumeingia makubaliano na wasambazaji wa mitungi ya gesi ya kupikia ambapo kwa mwaka huu 2024/2025 tunatoa mitungi zaidi ya laki nne kwa bei ya ruzuku ya asilimia 50," amesema.

Ameongeza kuwa majadiliano yanaendelea na watengenezaji wa majiko banifu ambapo kwa awamu ya kwanza majiko yapatayo 200,000 yatatolewa kwa bei ya ruzuku ya hadi asilimia 75.

Aidha alizungumzia suala la usambazaji wa umeme maeneo ya vijijini ambapo alisema hadi kufikia Desemba mwaka huu vijiji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimeunganishwa na umeme.

"Kwa sasa zaidi ya asilimia 98 ya vijiji vyote Tanzania Bara vimeunganishwa na umeme na sasa tumeanza kusambaza umeme vitongojini," amesema Mhandisi Mwijage.

Mhandisi Mwijage amesema Wakala unashiriki Kongamano la 10 la Jotoardhi kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya Nishati Jadidifu hasa ikizingatiwa kuwa Jotoardhi ni aina moja ya nishati jadidifu.

Amesema REA inafadhili miradi mbalimbali ya Nishati Jadidifu na kwamba kwa miradi ya upepo, jua na maporomoko ya maji Watanzania wengi wamejitokeza kushirikiana na Serikali kuitekeleza.

Hata hivyo amesema kwa Nishati ya Jotoardhi bado wananchi hawajawa na mwamko wa kutosha na kwamba kupitia kongamano na uhamasishaji unaofanywa na Serikali wanananchi watahamasika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top