Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Dkt. Mpango Atembelea Banda la REA
Frank A. Mugogo 278

Dkt. Mpango Atembelea Banda la REA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango amepongeza jitihada za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wananchi wanafikishiwa Nishati Safi ya Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Oktoba 23, 2024 Jijini Dar es Salaam alipotembelea Banda la REA katika Kongamano la 10 la Jotoardhi (ARGeo-C10).

Aidha ameielekeza REA kutazama namna ya kuweka ruzuku kwenye majiko yanayotumia nishati ya umeme kama inavyofanyika kwenye mitungi ya gesi na majiko banifu ili kuwawezesha wananchi wamudu gharama.

Alisema kwakuwa umeme umefika kila kona ya Nchi ni muhimu pia REA ikaandaa mpango maalum wa ruzuku katika majiko yanayotumia nishati ya umeme.

"Mmefanikisha kuweka ruzuku kwenye mitungi ya gesi na majiko banifu, mtazame namna ya kuwa na ruzuku kwenye majiko haya ya umeme ili kila mwananchi mwenye kuhitaji aweze kumudu gharama yake," alielekeza Mhe. Dkt. Mpango.

Awali akitoa maelelezo ya majukumu ya REA, Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi REA, Mhandisi Emanuel Yesaya alimueleza Makamu wa Rais, Mhe. Mpango kuwa Wakala unatekeleza programu mbalimbali ili kuhakikisha ifikapo mwaka 2034 asilima 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034).

Mhandisi Yesaya alisema Wakala umeingia makubaliano na wasambazaji wa mitungi ya gesi ambayo tayari inatolewa kwa bei ya ruzuku ya asilimia 50 katika mikoa yote Tanzania Bara ambapo kwa awamu ya kwanza mitungi ya 452,445 inatolewa.

Aidha alifafanua kuhusiana na ruzuku ya hadi asilimia 75 ambayo itatolewa katika majiko banifu ambapo alisema kwa kuanzia, takriban majiko 200,000 yatatolewa kwa bei hiyo ya ruzuku.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
1234
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Deadline for submission of Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts has been extended up to 15th September 2025.

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
567
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa Kitaifa, Ismail Ali Ussi amewahamasisha wananchi kuunga mkono kampeni ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya pamoja kuokoa mazingira.

Read more
8910
Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kukamilisha lengo la usambazaji Umeme katika Vijiji 12,318 Nchini na kwa umahiri wake katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
11121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top