Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama
Frank A. Mugogo 583

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme vijijini na Septemba 20 imetembelea na kukagua miradi hiyo katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
 
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenereali (mstaafu), Jacob Kingu amesema ziara hiyo ni muendelezo wa ziara za bodi hiyo kukagua usimamizi wa miradi ya nishati vijijini katika mikoa mbalimbali.
 
Mwenyekiti Kingu akiwa ameongozana na Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Radhia Msuya wamemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi katika Wilaya ya Kahama kuhakikisha anaongeza kasi na kukamilisha mradi kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika ili kila kijiji katika Mkoa wa Shinyanga kifikiwe na huduma ya nishati ya umeme ili dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata maendeleo iweze kutimia.
 
Kwa niaba ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameahidi kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi kumaliza mradi huo kwa wakati kama maelezo ya bodi yalivyotaka na kumtaka mkandarasi TonTan kuongeza watu wa kufanya kazi na kuhakikisha anawalipa stahiki zao kwa wakati ili wawe na morali ya kufanya kazi kwa bidi kuhakikisha vijiji vyote vilivyobaki vinakamilika ndani ya mwezi huu wa Septemba.
Ruanda.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«May 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
27282930123
45678
Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Read more
910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top