Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama
Frank A. Mugogo 38

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme vijijini na Septemba 20 imetembelea na kukagua miradi hiyo katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
 
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenereali (mstaafu), Jacob Kingu amesema ziara hiyo ni muendelezo wa ziara za bodi hiyo kukagua usimamizi wa miradi ya nishati vijijini katika mikoa mbalimbali.
 
Mwenyekiti Kingu akiwa ameongozana na Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Radhia Msuya wamemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi katika Wilaya ya Kahama kuhakikisha anaongeza kasi na kukamilisha mradi kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika ili kila kijiji katika Mkoa wa Shinyanga kifikiwe na huduma ya nishati ya umeme ili dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata maendeleo iweze kutimia.
 
Kwa niaba ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameahidi kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi kumaliza mradi huo kwa wakati kama maelezo ya bodi yalivyotaka na kumtaka mkandarasi TonTan kuongeza watu wa kufanya kazi na kuhakikisha anawalipa stahiki zao kwa wakati ili wawe na morali ya kufanya kazi kwa bidi kuhakikisha vijiji vyote vilivyobaki vinakamilika ndani ya mwezi huu wa Septemba.
Ruanda.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top