Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama
Frank A. Mugogo 354

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme vijijini na Septemba 20 imetembelea na kukagua miradi hiyo katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
 
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenereali (mstaafu), Jacob Kingu amesema ziara hiyo ni muendelezo wa ziara za bodi hiyo kukagua usimamizi wa miradi ya nishati vijijini katika mikoa mbalimbali.
 
Mwenyekiti Kingu akiwa ameongozana na Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Radhia Msuya wamemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi katika Wilaya ya Kahama kuhakikisha anaongeza kasi na kukamilisha mradi kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika ili kila kijiji katika Mkoa wa Shinyanga kifikiwe na huduma ya nishati ya umeme ili dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata maendeleo iweze kutimia.
 
Kwa niaba ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameahidi kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi kumaliza mradi huo kwa wakati kama maelezo ya bodi yalivyotaka na kumtaka mkandarasi TonTan kuongeza watu wa kufanya kazi na kuhakikisha anawalipa stahiki zao kwa wakati ili wawe na morali ya kufanya kazi kwa bidi kuhakikisha vijiji vyote vilivyobaki vinakamilika ndani ya mwezi huu wa Septemba.
Ruanda.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top