Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama
Frank A. Mugogo 72

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yakagua Utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Kahama

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme vijijini na Septemba 20 imetembelea na kukagua miradi hiyo katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
 
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenereali (mstaafu), Jacob Kingu amesema ziara hiyo ni muendelezo wa ziara za bodi hiyo kukagua usimamizi wa miradi ya nishati vijijini katika mikoa mbalimbali.
 
Mwenyekiti Kingu akiwa ameongozana na Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Radhia Msuya wamemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi katika Wilaya ya Kahama kuhakikisha anaongeza kasi na kukamilisha mradi kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika ili kila kijiji katika Mkoa wa Shinyanga kifikiwe na huduma ya nishati ya umeme ili dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata maendeleo iweze kutimia.
 
Kwa niaba ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameahidi kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi kumaliza mradi huo kwa wakati kama maelezo ya bodi yalivyotaka na kumtaka mkandarasi TonTan kuongeza watu wa kufanya kazi na kuhakikisha anawalipa stahiki zao kwa wakati ili wawe na morali ya kufanya kazi kwa bidi kuhakikisha vijiji vyote vilivyobaki vinakamilika ndani ya mwezi huu wa Septemba.
Ruanda.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top