Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA
Frank A. Mugogo 158

Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi wa umma.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameelekeza hayo Novemba 26, 2024 wakati wa mkutano na watumishi wote wa wakala.

"Majukumu yetu ya msingi ni kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini na Kuwezesha miradi ya Nishati Vijijini na majukumu haya tutayafanya kwa ufanisi endapo tutaendelea kuzingatia miongozo iliyopo," amesisitiza Mha. Saidy.

Amesema wakala unaendelea kufanya vizuri katika majukumu iliyokasimiwa na Serikali na ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kushirikiana kuhakikisha majukumu hayo yanatekelezwa kwa ufanisi na tija inapatikana.

Amepongeza watumishi kwa kuendelea kujituma na amesisitiza waendelee na moyo huo ili kutimiza dhamira ya Serikali.

"Serikali yetu inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetuamini katika kuwafikishia wananchi wake Nishati tusikubali kukwama kwa namna yoyote," ameelekeza.

Katika kikao hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali ya utekelezaji wa majuku yao sambamba na namna bora ya kuendelea kuboresha maeneo yao ya kazi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.

Read more
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top