Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA
Frank A. Mugogo 148

Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi wa umma.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameelekeza hayo Novemba 26, 2024 wakati wa mkutano na watumishi wote wa wakala.

"Majukumu yetu ya msingi ni kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini na Kuwezesha miradi ya Nishati Vijijini na majukumu haya tutayafanya kwa ufanisi endapo tutaendelea kuzingatia miongozo iliyopo," amesisitiza Mha. Saidy.

Amesema wakala unaendelea kufanya vizuri katika majukumu iliyokasimiwa na Serikali na ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kushirikiana kuhakikisha majukumu hayo yanatekelezwa kwa ufanisi na tija inapatikana.

Amepongeza watumishi kwa kuendelea kujituma na amesisitiza waendelee na moyo huo ili kutimiza dhamira ya Serikali.

"Serikali yetu inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetuamini katika kuwafikishia wananchi wake Nishati tusikubali kukwama kwa namna yoyote," ameelekeza.

Katika kikao hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali ya utekelezaji wa majuku yao sambamba na namna bora ya kuendelea kuboresha maeneo yao ya kazi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top