Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA
Frank A. Mugogo 138

Zingatieni Sheria Kanuni na Taratibu- DG REA

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi wa umma.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameelekeza hayo Novemba 26, 2024 wakati wa mkutano na watumishi wote wa wakala.

"Majukumu yetu ya msingi ni kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini na Kuwezesha miradi ya Nishati Vijijini na majukumu haya tutayafanya kwa ufanisi endapo tutaendelea kuzingatia miongozo iliyopo," amesisitiza Mha. Saidy.

Amesema wakala unaendelea kufanya vizuri katika majukumu iliyokasimiwa na Serikali na ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kushirikiana kuhakikisha majukumu hayo yanatekelezwa kwa ufanisi na tija inapatikana.

Amepongeza watumishi kwa kuendelea kujituma na amesisitiza waendelee na moyo huo ili kutimiza dhamira ya Serikali.

"Serikali yetu inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetuamini katika kuwafikishia wananchi wake Nishati tusikubali kukwama kwa namna yoyote," ameelekeza.

Katika kikao hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali ya utekelezaji wa majuku yao sambamba na namna bora ya kuendelea kuboresha maeneo yao ya kazi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top