Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Majiko ya Gesi 19,530 Kusambazwa kwa Bei ya Ruzuku Mkoani Kilimanjaro
Frank A. Mugogo 494

Majiko ya Gesi 19,530 Kusambazwa kwa Bei ya Ruzuku Mkoani Kilimanjaro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatarajia kusambaza jumla ya majiko ya gesi (LPG) ya kilo sita 19,530 yanayotolewa kwa bei ya ruzuku ya 50% Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034. 

Hayo yameelezwa Desemba 6, 2024 na Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi REA, Mhandisi Emanuel Yesaya Mkoani Kilimanjaro wakati wa kutambulisha mradi wa kusambaza majiko ya gesi kwa bei ya ruzuku sambamba na kumtambulisha msambazaji ambaye ni Kampuni ya Lake Gas katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. 

"Tumeanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza majiko ya gesi kwa bei ya ruzuku tupo hapa kutambulisha rasmi mradi huu unaogharimu kiasi cha shilingi milioni 407 kwa mkoa huu na pia  kumtambulisha msambazaji katika mkoa huu ambaye ni Kampuni ya Lake Gas," amesema Mhandisi Yesaya. 

Mhandisi Yesaya amesema REA imejipanga kutekeleza azma ya Serikali inayoongozwa na Rais. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha ifikapo mwaka 2034; 80% ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia. 

Akizungumza wakati wa kupokea mradi huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Nzowa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, aliipongeza REA kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutekeleza dhamira na ajenda kuu ya Rais. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.
 
"Tunashuhudia REA inatekeleza kwa vitendo dhamira ya Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanatumia nishati safi kupikia na wanaachana na matumizi ya kuni na mkaa ili kulinda kuhifadhi mazingira na pia kulinda afya," amesema. 

Ametoa wito kwa wananchi mkoani humo kuchangamkia fursa hiyo iliyotolewa na Serikali kupitia REA hasa ikizingatiwa kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yanaokoa gharama na muda ambao mwananchi anaweza kutumia kufanya shughuli nyingine za kiuchumi lakini pia ni rafiki wa mazingira na afya kwa mtumiaji.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi kwa ujumla, Mhandisi Yesaya amesema kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025, jumla ya majiko ya gesi 452,445 ya kilo sita yenye thamani ya shilingi bilioni 10 yatasambazwa kote nchini kwa bei ya ruzuku ya asimilia 50.
 
Mhandisi Yesaya ameeleza kuwa mbali ya mradi huo wa usambazaji wa majiko ya gesi; REA vilevile inaandaa mradi wa kusambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku ambapo alisema jumla ya majiko 200,000 yatasambazwa kwa bei ya ruzuku ya 75% hadi 85% kwa maeneo ya vijijini kote nchini. 

Amesema lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa kulingana na hali yake ya kiuchumi ili kufikia lengo kuu la mkakati la kufikisha 80% ya watanzania watakaotumia nishati safi na iloyo bora ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«November 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
101112131415
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Read more
16
Watumishi REA Wapongezwa

Watumishi REA Wapongezwa

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wapongezwa kwa kujituma na kufanya kazi kwa bidii hali iliyopelekea mafanikio makubwa ya Wakala huo ikiwamo kufikisha umeme katika Vijiji vyote vya Tanzania Bara.

Read more
171819
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemuapisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi pamoja na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Salome Wycliffe Makamba wakati wa Hafla ya kuwaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma Novemba 18, 2025

Read more
20212223
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top