Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA , BUTIAMA, MKOA WA MARA
Admin.Frank Mugogo 10297

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA , BUTIAMA, MKOA WA MARA

Tarehe 5 Juni, kila mwaka Watanzania wanaungana na mataifa mengine kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani. Kitaifa maadhimisho haya yalifanyika katika Kijiji cha Butiama, Mkoani Mara ambako Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ulishiriki.

Katika maadhimisho hayo, Wakala ulipata fursa ya kuonesha mpango wake wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara na mikoa mingine pamoja na kupokea maoni na mahitaji ya wananchi wa Mkoa wa Mara ambao hawajafikiwa na huduma ya umeme.

Katika kuonesha uhalisia wa miradi ambayo inatekelezwa na Wakala, wakandarasi na waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini walishiriki katika maadhimisho hayo kupitia banda la Wakala ambao ni pamoja na:

i. DERM Electric – Mkandarasi wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara (Mradi Kabambe Awamu ya II);

ii. Angelique International Ltd – Mkandarasi wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara (Mradi Kabambe Awamu ya III, kipengele cha Densification); na

iii. PowerGen Renewable Energy – Mradi wa umeme-jua (Solar Mini grid - LRTC 2014) katika eneo la Raranya, mkoani Mara.

Madhumuni ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ni kuhamasisha jamii kuelewa masuala yahusuyo mazingira na kuchukua hatua za kuhifadhi na kulinda mazingira. Kauli Mbiu iliyoongoza maadhimisho haya kitaifa ni “Hifadhi ya Mazingira: Muhimili kwa Tanzania ya viwanda”, lengo likiwa ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira wakati tunapokuza maendeleo ya viwanda nchini.

Wakati wa maadhmisho hayo, banda la Wakala wa Nishati Vijijini lilitembelewa na wageni mbalimbali ikiwa ni pamoja na mgeni rasmi wakati wa kilele cha maadhmisho hayo ambaye alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan. Pia wakazi wa kijiji cha Butiama, vitongoji mbalimbali na maeneo mengine ya Mkoa wa Mara walitembelea banda la Wakala wakiwa na shauku ya kujua utekelezwaji wa miradi mbalimbali.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top