Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi
Mohamed Saif 271

Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Kusambazwa wilaya zote za Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruzuku ya shilingi 7,500 yanayosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kulinda afya, kuokoa misitu na kuhifadhi mazingira.

Ametoa rai hiyo Desemba 18, 2025 Mkoani Katavi wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusambaza majiko banifu ya ruzuku yapatayo 3,126 mkoani humo unaotekelezwa na Kampuni ya Tango Energy Ltd ya Jijini Dar es Salaam unaoratibiwa na kusimamiwa na REA wenye thamani ya shilingi milioni 156.3 ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034).

“Nitoe wito kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi, majiko haya ni kwa ajili yenu na yameuzwa kwa bei ya ruzuku kwa maana ya kwamba Serikali imelipia zaidi ya shilingi 50,000 lakini mwananchi analipia shilingi 7,500 pekee, naomba mchangamkie fursa hii,” amesisitiza Mhe, Mrindoko.

Mhe. Mrindoko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amejielekeza katika kuhakikisha kwamba wananchi wote wanatumia nishati safi ya kupikia.

Alisisitiza wananchi wa Katavi kuhakikisha maono na maelekezo ya Rais ya kuendelea kutunza misitu yanatekelezwa na kwamba kupitia mradi wa kusambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku utawezesha uhifadhi wa misitu.

“Tunamshukuru Rais na tunamhakikishia kwamba afua zote zinazohusiana na utunzaji wa mazingira, utunzaji wa misitu kwa kusaidiana na Wakuu wa Wilaya na watendaji tutahakikisha jambo hili linafanikiwa kikamilifu ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa,” alisema Mhe. Mrindoko.

Akitambulisha mradi, Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka REA, Dkt. Joseph Sambali alisema majiko hayo yatauzwa kwa shilingi 7,500 badala ya shilingi 59,000 kwakuwa Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya 85% sambamba na kuondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika majiko hayo ili kumpa unafuu mwananchi.

“Kabla ya ruzuku jiko moja lilikuwa likiuzwa kwa shilingi 59,000 na baada ya Serikali kuweka ruzuku likauzwa kwa shilingi 8,850 lakini sasa baada pia ya kuondoa kodi ya VAT jiko moja hapa Katavi litauzwa kwa shilingi 7,500 pekee," alibainisha Dkt. Sambali.

Alisema katika kila Wilaya majiko banifu 1,042 yatasambazwa ambayo jumla yake ni majiko 3,126 ambapo alizitaja wilaya hizo kuwa ni Mpanda, Mlele na Tanganyika.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tango Energy Ltd, Musa Msofe alisema wamejipanga ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwamba majiko hayo yatauzwa kwa bei ya ruzuku kwa mwananchi mwenye kitambulisho cha Taifa (NIDA) na kwamba majiko hayo yana udhamini (warranty) wa mwaka mmoja.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top