Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma
Issa Sabuni 165

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Ni tuzo ya ubora katika kushughulikia malalamiko kwa Wananchi na kutoa mrejesho

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

Tuzo hiyo imetolewa usiku wa tarehe 16 Desemba, 2025 na Bwana, Shariff Shariff; Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kupokelewa na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi, Jones Olotu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA katika ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya utoaji wa tuzo hizo, imeandaliwa na Taasisi ya Tanzania Professional Skills and Innovation Awards (TPSIA) kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta binafsi ili kutambua na kuthamini mchango na jitihada za Taasisi za Umma kwa maendeleo ya Taifa.

Tuzo hizo zimepewa jina la *Tuzo za Ubunifu kwenye Utumishi wa Umma* (Public Service and Innovation Awards) ambapo zaidi ya Taasisi 300 za Serikali zimeshindanishwa katika makundi 29 ambapo REA imekuwa mshindi katika Kundi la 28 la Taasisi Bora iliyoshughulikia Malalamiko ya Wateja katika Utoaji wa Huduma kwa Umma mwaka 2025 hususan huduma za nishati vijijini (Customer Feedback and Complain Handling Award, 2025).

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mhandisi Olotu amesema, imekuja katika wakati sahihi ambao Wakala imekamilisha jukumu la kusambaza umeme kwenye vijiji vyote Tanzania Bara (Vijiji 12,318); umeme umesambazwa kwenye jumla ya vitongoji 39,003 kati ya vitongoji vyote 64,359 pamoja na kusambaza teknolojia za nishati safi ya kupikia kwa Watanzania ambapo zaidi ya mitungi ya gesi ya kupikia (LPG) laki nane (800,000) kwa bei ya ruzuku (Nusu Bei).

“Kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu na Menejimenti ya REA; tunawashukuru Waandaaji wa tuzo hizi kwa kutambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na REA katika kusambaza nishati bora vijijini, tuzo hii imekuja katika kipindi fasaha, ambapo tumefikisha umeme kwenye vijiji vyote 12,318; tumefikisha umeme kwenye vitongoji 39,003 kati ya vitongoji vyote 64,359, kipindi ambacho tumehamasisha na kusambaza nishati safi ya kupikia, ambapo zaidi ya mitungi ya gesi laki nane (800,000) imesambazwa kwenye wilaya zote 139 za Tanzania Bara, tumefanya hivyo kwa kuwa, tunaamini umeme ni kichecheo kikubwa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa Wananchi wa vijijini.” Amekaririwa, Mhandisi, Olotu.

MWISHO!!!

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top