Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma
Issa Sabuni 80

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Ni tuzo ya ubora katika kushughulikia malalamiko kwa Wananchi na kutoa mrejesho

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

Tuzo hiyo imetolewa usiku wa tarehe 16 Desemba, 2025 na Bwana, Shariff Shariff; Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kupokelewa na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi, Jones Olotu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA katika ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya utoaji wa tuzo hizo, imeandaliwa na Taasisi ya Tanzania Professional Skills and Innovation Awards (TPSIA) kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta binafsi ili kutambua na kuthamini mchango na jitihada za Taasisi za Umma kwa maendeleo ya Taifa.

Tuzo hizo zimepewa jina la *Tuzo za Ubunifu kwenye Utumishi wa Umma* (Public Service and Innovation Awards) ambapo zaidi ya Taasisi 300 za Serikali zimeshindanishwa katika makundi 29 ambapo REA imekuwa mshindi katika Kundi la 28 la Taasisi Bora iliyoshughulikia Malalamiko ya Wateja katika Utoaji wa Huduma kwa Umma mwaka 2025 hususan huduma za nishati vijijini (Customer Feedback and Complain Handling Award, 2025).

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mhandisi Olotu amesema, imekuja katika wakati sahihi ambao Wakala imekamilisha jukumu la kusambaza umeme kwenye vijiji vyote Tanzania Bara (Vijiji 12,318); umeme umesambazwa kwenye jumla ya vitongoji 39,003 kati ya vitongoji vyote 64,359 pamoja na kusambaza teknolojia za nishati safi ya kupikia kwa Watanzania ambapo zaidi ya mitungi ya gesi ya kupikia (LPG) laki nane (800,000) kwa bei ya ruzuku (Nusu Bei).

“Kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu na Menejimenti ya REA; tunawashukuru Waandaaji wa tuzo hizi kwa kutambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na REA katika kusambaza nishati bora vijijini, tuzo hii imekuja katika kipindi fasaha, ambapo tumefikisha umeme kwenye vijiji vyote 12,318; tumefikisha umeme kwenye vitongoji 39,003 kati ya vitongoji vyote 64,359, kipindi ambacho tumehamasisha na kusambaza nishati safi ya kupikia, ambapo zaidi ya mitungi ya gesi laki nane (800,000) imesambazwa kwenye wilaya zote 139 za Tanzania Bara, tumefanya hivyo kwa kuwa, tunaamini umeme ni kichecheo kikubwa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa Wananchi wa vijijini.” Amekaririwa, Mhandisi, Olotu.

MWISHO!!!

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top