Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)
Admin.Frank Mugogo 13086

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)

Waziri wa Nishati, Mh. Dk. Medard Kalemani amezindua Bodi ya Nishati Vijijini (REB), leo tarehe 18 Februari, 2019 itakayosimamia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kutoa maelekezo mbalimbali yatakayopelekea kazi ya usambazaji umeme vijijini kufanyika kwa kasi na ufanisi..

Uzinduzi wa Bodi hiyo umefanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Nishati akiwemo Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Mgalu; Katibu Mkuu, Dkt. Hamisi Mwinyimvua; Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga; Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Raphael Nombo; Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga na watendaji wengine kutoka Wizara na Wakala wa Nishati Vijijini.

Mh. Waziri wa Nishati alieleza kuwa, Bodi mpya ya Nishati Vijijini imeundwa kufuatia kuvunjwa kwa Bodi iliyopita tarehe 12 Novemba, 2018 kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kushindwa kusimamia vizuri Wakala wa Nishati Vijijini.

Wajumbe wapya wa Bodi hiyo ni kama ifuatavyo:

Dr. Andrew Marceline Komba - Mjumbe
Ms. Dailin Leonard Mgweno - Mjumbe
Mr. Oswald Martin Urasa - Mjumbe
Mr. Henry Mwatwinzwa Mwimbe - Mjumbe
Eng. Styden Rwebangira - Mjumbe
Mr. Louis Passian Accaro - Mjumbe
Mr. Francis M. Songela - Mjumbe

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top