Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)
Admin.Frank Mugogo 12503

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)

Waziri wa Nishati, Mh. Dk. Medard Kalemani amezindua Bodi ya Nishati Vijijini (REB), leo tarehe 18 Februari, 2019 itakayosimamia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kutoa maelekezo mbalimbali yatakayopelekea kazi ya usambazaji umeme vijijini kufanyika kwa kasi na ufanisi..

Uzinduzi wa Bodi hiyo umefanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Nishati akiwemo Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Mgalu; Katibu Mkuu, Dkt. Hamisi Mwinyimvua; Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga; Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Raphael Nombo; Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga na watendaji wengine kutoka Wizara na Wakala wa Nishati Vijijini.

Mh. Waziri wa Nishati alieleza kuwa, Bodi mpya ya Nishati Vijijini imeundwa kufuatia kuvunjwa kwa Bodi iliyopita tarehe 12 Novemba, 2018 kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kushindwa kusimamia vizuri Wakala wa Nishati Vijijini.

Wajumbe wapya wa Bodi hiyo ni kama ifuatavyo:

Dr. Andrew Marceline Komba - Mjumbe
Ms. Dailin Leonard Mgweno - Mjumbe
Mr. Oswald Martin Urasa - Mjumbe
Mr. Henry Mwatwinzwa Mwimbe - Mjumbe
Eng. Styden Rwebangira - Mjumbe
Mr. Louis Passian Accaro - Mjumbe
Mr. Francis M. Songela - Mjumbe

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top