Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)
Admin.Frank Mugogo 12509

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI MPYA YA NISHATI VIJIJINI (REB)

Waziri wa Nishati, Mh. Dk. Medard Kalemani amezindua Bodi ya Nishati Vijijini (REB), leo tarehe 18 Februari, 2019 itakayosimamia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kutoa maelekezo mbalimbali yatakayopelekea kazi ya usambazaji umeme vijijini kufanyika kwa kasi na ufanisi..

Uzinduzi wa Bodi hiyo umefanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Nishati akiwemo Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Mgalu; Katibu Mkuu, Dkt. Hamisi Mwinyimvua; Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga; Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Raphael Nombo; Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga na watendaji wengine kutoka Wizara na Wakala wa Nishati Vijijini.

Mh. Waziri wa Nishati alieleza kuwa, Bodi mpya ya Nishati Vijijini imeundwa kufuatia kuvunjwa kwa Bodi iliyopita tarehe 12 Novemba, 2018 kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kushindwa kusimamia vizuri Wakala wa Nishati Vijijini.

Wajumbe wapya wa Bodi hiyo ni kama ifuatavyo:

Dr. Andrew Marceline Komba - Mjumbe
Ms. Dailin Leonard Mgweno - Mjumbe
Mr. Oswald Martin Urasa - Mjumbe
Mr. Henry Mwatwinzwa Mwimbe - Mjumbe
Eng. Styden Rwebangira - Mjumbe
Mr. Louis Passian Accaro - Mjumbe
Mr. Francis M. Songela - Mjumbe

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania
Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top