Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA
Frank A. Mugogo 360

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma Mei 16, 2025 na Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Nishati Tanzania kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Rhonda Antoine wakati wa kikao cha Ujumbe kutoka WB na REA kujadili hatua za utekelezwaji wa miradi ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, uendelezaji wa miradi ya nishati mbadala na mradi wa kusambaza umeme vitongojini kote nchini.

"Tunaipongeza REA; tunaahidi kuendeleza ushirikiano wetu kwa kazi kubwa inayofanya, tumeridhishwa na hatua mbalimbali zinazochukuliwa wakati wote wa kutekeleza miradi, vigezo vimezingatiwa," alisema Dkt. Antoine

Akizungumza katika kikao hicho kilichokutanisha viongozi na wataalam kutoka REA na ujumbe huo wa Benki ya Dunia, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy alishukuru ushirikiano unaotolewa na benki hiyo katika kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali inayosimamiwa na REA.

"Tunashirikiana kwa karibu na Wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo WB katika kufanikisha utekelezaji wa miradi tunayoisimamia kwa mustakabali mzima wa maendeleo ya Watanzania wote," alisema Mhandisi Saidy.

Alisema Serikali imeipa jukumu REA kutumia nyenzo na maarifa mbalimbali kuhakikisha umeme unafika kwenye vitongoji vyote nchini sambamba na kuhakikisha mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unafanikiwa kwa kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Aliuhakikishia ujumbe huo kuwa REA itaendelea kusimamia vyema miradi iliyochini yake kama ambavyo miongozo mbalimbali ya WB inavyoelekeza.

Aidha, ujumbe huo wa WB uliipongeza REA kwa kuzingatia dhana ya usawa wa kijinsia wakati wote wa utekelezaji wa miradi pamoja na namna ambavyo inashirikiana na wadau kutoka Sekta Binafsi kutekeleza miradi.

Kikao hicho ni taratibu iliyowekwa na Benki ya Dunia kujadili hatua za utekelezaji wa miradi inayoifadhili na kufuatilia maendeleo ya utekelezwaji wake.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top