Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA
Frank A. Mugogo 107

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma Mei 16, 2025 na Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Nishati Tanzania kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Rhonda Antoine wakati wa kikao cha Ujumbe kutoka WB na REA kujadili hatua za utekelezwaji wa miradi ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, uendelezaji wa miradi ya nishati mbadala na mradi wa kusambaza umeme vitongojini kote nchini.

"Tunaipongeza REA; tunaahidi kuendeleza ushirikiano wetu kwa kazi kubwa inayofanya, tumeridhishwa na hatua mbalimbali zinazochukuliwa wakati wote wa kutekeleza miradi, vigezo vimezingatiwa," alisema Dkt. Antoine

Akizungumza katika kikao hicho kilichokutanisha viongozi na wataalam kutoka REA na ujumbe huo wa Benki ya Dunia, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy alishukuru ushirikiano unaotolewa na benki hiyo katika kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali inayosimamiwa na REA.

"Tunashirikiana kwa karibu na Wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo WB katika kufanikisha utekelezaji wa miradi tunayoisimamia kwa mustakabali mzima wa maendeleo ya Watanzania wote," alisema Mhandisi Saidy.

Alisema Serikali imeipa jukumu REA kutumia nyenzo na maarifa mbalimbali kuhakikisha umeme unafika kwenye vitongoji vyote nchini sambamba na kuhakikisha mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unafanikiwa kwa kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Aliuhakikishia ujumbe huo kuwa REA itaendelea kusimamia vyema miradi iliyochini yake kama ambavyo miongozo mbalimbali ya WB inavyoelekeza.

Aidha, ujumbe huo wa WB uliipongeza REA kwa kuzingatia dhana ya usawa wa kijinsia wakati wote wa utekelezaji wa miradi pamoja na namna ambavyo inashirikiana na wadau kutoka Sekta Binafsi kutekeleza miradi.

Kikao hicho ni taratibu iliyowekwa na Benki ya Dunia kujadili hatua za utekelezaji wa miradi inayoifadhili na kufuatilia maendeleo ya utekelezwaji wake.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top