Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme
Admin.Frank Mugogo 7276

Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo amevipongeza viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa uzalishaji wa vifaa kwa kiwango kikubwa unaochochea ukuaji wa sekta ya nishati nchini.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ilifanya ziara ya kutembelea viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Njombe na Iringa ili kujionea shughuli za uzalishaji vifaa hivyo.
Katika ziara hiyo, wamiliki wa viwanda vya vifaa vya umeme wameahidi kuendelea kuzalisha vifaa hivyo kwa kiwango kikubwa ili kukidhi mahitaji ya miradi ya umeme nchini.

Wakili Kalolo alisema ameridhishwa na kasi ya uzalishaji wa vifaa katika viwanda hivyo na kusisitiza umuhimu wake katika kufanikisha kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijijni ambayo inaendelea nchini, ambapo mpaka sasa ni vijiji 7400 kati ya 12,268 vimeunganishwa na huduma ya umeme.
“Ziara hii imetusaidia kujua changamoto wanazokumbana nazo wazalishaji wa vifaa vya umeme, lakini pia naweza kuthibitisha uwezo wao baada ya kutembelea viwanda hivi, ni wazi kwamba suala la nguzo za umeme tunajitosheleza kwa viwanda vyetu, suala la mita na waya sio changamoto, vyote vinazalishwa ndani ya nchi”, aliongeza Wakili Kalolo.

Pia Wakili Kalolo amewapongeza wamiliki wa viwanda hivyo kwa kuajiri wafanyakazi wazawa kwa wingi na kuwataka kuendelea kuongeza wafanyakazi wanaopatikana hapa hapa nchini Tanzania. Wakili Kalolo aliongeza kusema kuwa, Serikali imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuhakikisha kuwa juhudi za Rais John Magufuli kwamba Serikali itafikia uchumi wa kati kufikia Mwaka 2025.

Akielezea umuhimu wa viwanda hivyo katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga amesema watengenezaji wa vifaa vinavyotumika katika miradi ya umeme, kama vile mita, waya, transfoma, nguzo na vingine vingi ni wadau muhimu sana katika kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo vijijini kupitia nishati ya umeme.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«May 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top