Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme
Admin.Frank Mugogo 7882

Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo amevipongeza viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa uzalishaji wa vifaa kwa kiwango kikubwa unaochochea ukuaji wa sekta ya nishati nchini.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ilifanya ziara ya kutembelea viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Njombe na Iringa ili kujionea shughuli za uzalishaji vifaa hivyo.
Katika ziara hiyo, wamiliki wa viwanda vya vifaa vya umeme wameahidi kuendelea kuzalisha vifaa hivyo kwa kiwango kikubwa ili kukidhi mahitaji ya miradi ya umeme nchini.

Wakili Kalolo alisema ameridhishwa na kasi ya uzalishaji wa vifaa katika viwanda hivyo na kusisitiza umuhimu wake katika kufanikisha kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijijni ambayo inaendelea nchini, ambapo mpaka sasa ni vijiji 7400 kati ya 12,268 vimeunganishwa na huduma ya umeme.
“Ziara hii imetusaidia kujua changamoto wanazokumbana nazo wazalishaji wa vifaa vya umeme, lakini pia naweza kuthibitisha uwezo wao baada ya kutembelea viwanda hivi, ni wazi kwamba suala la nguzo za umeme tunajitosheleza kwa viwanda vyetu, suala la mita na waya sio changamoto, vyote vinazalishwa ndani ya nchi”, aliongeza Wakili Kalolo.

Pia Wakili Kalolo amewapongeza wamiliki wa viwanda hivyo kwa kuajiri wafanyakazi wazawa kwa wingi na kuwataka kuendelea kuongeza wafanyakazi wanaopatikana hapa hapa nchini Tanzania. Wakili Kalolo aliongeza kusema kuwa, Serikali imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuhakikisha kuwa juhudi za Rais John Magufuli kwamba Serikali itafikia uchumi wa kati kufikia Mwaka 2025.

Akielezea umuhimu wa viwanda hivyo katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga amesema watengenezaji wa vifaa vinavyotumika katika miradi ya umeme, kama vile mita, waya, transfoma, nguzo na vingine vingi ni wadau muhimu sana katika kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo vijijini kupitia nishati ya umeme.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top