Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 155

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Wito huo umetolewa Oktoba 10, 2024 Wilayani Bukombe na Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage wakati wa Semina maalum ya Nishati  Safi ya Kupikia kwa wakazi wa Wilaya hiyo.

"Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya Nishati Safi ya kupikia na anafanya kila linalowezekana  kuhakikisha kila mwananchi anapata bidhaa za Nishati Safi za kupikia kwa gharama nafuu", alisema Mhandisi Mwijage.

Akizungumza wakati wa Semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Mhe. Paskasi Muragili alimshukuru Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruzuku kwenye bidhaa za nishati safi za kupikia suala ambalo alisema linakwenda kuimarisha afya za wananchi sanjari na kuhifadhi mazingira ambayo kwa kiasi kikubwa alisema yameathiriwa na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

"Leo ni siku ya kihistoria kwa wakazi wa Bukombe, tunakwenda kupokea mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku na hizi ni jitihada za Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza," alisema Mhe. Muragili. 

Aliwasihi wananchi wote watakaojipatia mitungi hiyo kuhakikisha inapomalizika wanajaza ili kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia na si kurejea katika matumizi ya kuni na mkaa.

Akizungumza wakati wa Semina hiyo, Mhandisi Mwijage alisema Wakala umepewa jukumu la kuhakikisha bidhaa za nishati safi za kupikia zinafika katika kila pembe ya nchi ili kumuwezesha kila mwananchi kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama.

"Serikali kupitia REA imeanza na itaendelea kutoa ruzuku kwa bidhaa za nishati safi za kupikia lengo ikiwa ni kuhakikisha hakuna mwananchi anaachwa nyuma," alisema.

Mhandisi Advera alisema kwa bidhaa za mitungi ya gesi (LPG) Serikali imeingia makubaliano na watoa huduma ya kusambaza mitungi na katika mikoa yoye nchini ambapo kwa awamu hii kiasi cha mitungi 452,445 itatolewa kwa bei ya ruzuku katika kila Mkoa

"Kwa hapa Bukombe, mtoa huduma atakayesambaza mitungi ni Kampuni ya Manjis ambapo mitungi hii ya kilo sita ikiwa kamili na kichomeo na figa  itatolewa kwa shilingi 17,500 tu ambayo ni nusu bei, sawa na asilimia 50 tu ya gharama ili wananchi waweze kumudu gharama za nishati ya kupikia" Asilimia nyingine 50 inalipwa na serikali, alisema Mhandisi Mwijage.

Aliongeza kuwa upo mradi wa majiko banifu ambao wancho watachangia shingili elfu 5 hadi 15, na kwa sasa mradi huo upo katika hatua za uandaaji wa mikataba. Jumla ya majiko 200,000 yatasambazwa nchi nzima. Miradi mingine iliyotajwa ni pamoja na usambazaji wa gesi asilia,kuongeza uzalishaji wa mkaa  Mbadala,kuwezesha taasisi zinazolisha watu zaidi ya watu 100 kutumia nishati safi pamoja na kutoa elimu kwa umma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe, Mhe Yusuph Yusuph alipongeza uwepo wa semina hiyo ambayo alisema itaongeza uelewa miongoni mwa wanamchi kuhusiana na suala zima la nishati safi za kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top