Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 140

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Wito huo umetolewa Oktoba 10, 2024 Wilayani Bukombe na Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage wakati wa Semina maalum ya Nishati  Safi ya Kupikia kwa wakazi wa Wilaya hiyo.

"Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya Nishati Safi ya kupikia na anafanya kila linalowezekana  kuhakikisha kila mwananchi anapata bidhaa za Nishati Safi za kupikia kwa gharama nafuu", alisema Mhandisi Mwijage.

Akizungumza wakati wa Semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Mhe. Paskasi Muragili alimshukuru Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruzuku kwenye bidhaa za nishati safi za kupikia suala ambalo alisema linakwenda kuimarisha afya za wananchi sanjari na kuhifadhi mazingira ambayo kwa kiasi kikubwa alisema yameathiriwa na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

"Leo ni siku ya kihistoria kwa wakazi wa Bukombe, tunakwenda kupokea mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku na hizi ni jitihada za Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza," alisema Mhe. Muragili. 

Aliwasihi wananchi wote watakaojipatia mitungi hiyo kuhakikisha inapomalizika wanajaza ili kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia na si kurejea katika matumizi ya kuni na mkaa.

Akizungumza wakati wa Semina hiyo, Mhandisi Mwijage alisema Wakala umepewa jukumu la kuhakikisha bidhaa za nishati safi za kupikia zinafika katika kila pembe ya nchi ili kumuwezesha kila mwananchi kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama.

"Serikali kupitia REA imeanza na itaendelea kutoa ruzuku kwa bidhaa za nishati safi za kupikia lengo ikiwa ni kuhakikisha hakuna mwananchi anaachwa nyuma," alisema.

Mhandisi Advera alisema kwa bidhaa za mitungi ya gesi (LPG) Serikali imeingia makubaliano na watoa huduma ya kusambaza mitungi na katika mikoa yoye nchini ambapo kwa awamu hii kiasi cha mitungi 452,445 itatolewa kwa bei ya ruzuku katika kila Mkoa

"Kwa hapa Bukombe, mtoa huduma atakayesambaza mitungi ni Kampuni ya Manjis ambapo mitungi hii ya kilo sita ikiwa kamili na kichomeo na figa  itatolewa kwa shilingi 17,500 tu ambayo ni nusu bei, sawa na asilimia 50 tu ya gharama ili wananchi waweze kumudu gharama za nishati ya kupikia" Asilimia nyingine 50 inalipwa na serikali, alisema Mhandisi Mwijage.

Aliongeza kuwa upo mradi wa majiko banifu ambao wancho watachangia shingili elfu 5 hadi 15, na kwa sasa mradi huo upo katika hatua za uandaaji wa mikataba. Jumla ya majiko 200,000 yatasambazwa nchi nzima. Miradi mingine iliyotajwa ni pamoja na usambazaji wa gesi asilia,kuongeza uzalishaji wa mkaa  Mbadala,kuwezesha taasisi zinazolisha watu zaidi ya watu 100 kutumia nishati safi pamoja na kutoa elimu kwa umma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe, Mhe Yusuph Yusuph alipongeza uwepo wa semina hiyo ambayo alisema itaongeza uelewa miongoni mwa wanamchi kuhusiana na suala zima la nishati safi za kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top