Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige
Frank A. Mugogo 627

Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kukamilisha lengo la usambazaji Umeme katika Vijiji 12,318 Nchini na kwa umahiri wake katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Agosti 22, 2025 Jijini Dodoma wakati wa hafla ya kukabidhi majiko yanayotumia Nishati Safi kwa Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

"REA mmefanya kazi kubwa, tunawapongeza kwa kuibeba vyema ajenda ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya Nishati Safi ya Kupikia sambamba na kukamilisha kwa wakati lengo la kufikisha umeme katika vijiji vyote 12,318 na sasa mnasambaza umeme vitongojini," alipongeza Mhe. Dkt.Biteko.

Aliipongeza Bodi ya Nishati Vijijini (REB) chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu kwa umahiri wake katika katika kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kasi na viwango sambamba na kumpongeza Mtendaji Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy kwa kusimamia vyema watendaji walio chini yake.

Alibainisha kuwa Wizara ya Nishati inao utaratibu wa kupima utendaji wa kila taasisi inayoisimamia na kwamba REA ni taasisi ambayo imefanya vizuri mara tatu mfululizo kuatika tathmini hiyo ya utendaji wa taasisi ambayo hufanyika kila baada ya miezi mitatu.

"Katika robo ya kwanza ya upimaji wa utendaji REA ilishinda nafasi ya kwanza, robo iliyofuatia REA ilichukua nafasi ya pili na robo hii iliyomalizika hivi karibuni REA imeshika nafasi ya kwanza kwa taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati, kazi mnayofanya imewezekana kwasababu ya utulivu wa taasisi, mnayo Bodi nzuri na uongozi mzuri," alibainisha Mhe. Dkt. Biteko.

Aliongeza kuwa miradi yote inayosimamiwa na REA inakamilika kwa wakati na kwa ubora mzuri na kwamba hajawahi kupokea malalamiko yoyote kutoka kwa wafadhili wa miradi na mara zote wamekuwa wakimpatia sifa njema za utendaji wa Wakala.

"Nampongeza Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy kwa uongozi wake amewafanya watumishi wa REA wajione wa daraja la juu, hajawagawa kwa makundi hana wapambe ndio maana huwezi kusikia kelele, tuendelee kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia vyema miradi tuliyokabidhiwa," alisema Mhe.Dkt. Biteko.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu alisema Wakala unaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo. 

"Ombi langu zoezi hili itapendeza na kuleta matokeo chanya endapo taasisi zote zitatoa majiko haya kwa watumishi; hii italeta chachu kwa Wizara zingine na taasisi mbalimbali kufanya vivyo hivyo na itaongeza kasi ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais ya kuhakikisha 80% ya Watanzania wanahamia kutumia Nishati Safi ifikapo mwaka 2034 na hili linawezekana," alisema Balozi Kingu.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Nishati Safi ya Kupikia, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy alimshukuru Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa miongozo yake ya namna bora ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo la 80% ifikapo mwaka 2034.

Mhandisi Saidy aliainisha mikakati mbalimbali inayoendelea kutekelezwa kupitia REA na alitaja baadhi ya miradi ikiwemo kujenga mifumo ya gesi asilia Lindi na Pwani na kwamba hadi sasa wananchi 460 wamefikiwa kati ya 980 waliolengwa, kufunga mifumo katika Jeshi la Magereza ambapo magereza yote 129 yamefikiwa sambamba na kufunga mifumo katika kambi 22 za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Mbali na miradi hiyo, Mhandisi Saidy alisema REA imeliwezesha Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kiasi cha shilingi bilioni 3 kujenga mtambo wa kuzalisha mkaa mbadala maarufu kama 'rafiki briquettes', majiko banifu 200,000 vijijini kusaidia wananchi ambao ni ngumu kufikiwa na nishati safi zingine.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top