Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
JAPANI YAVUTIWA NA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI
Host 12576

JAPANI YAVUTIWA NA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

Serikali ya Japani imekiri kuvutiwa na kuhamasishwa na fursa za uwekezaji zilizopo hapa nchini hususan katika sekta ya nishati na imeonesha nia ya kuwekeza katika sekta hiyo.

Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan Mhe. Toshimitsu Motegi aliyasema hayo hivi karibuni alipofanya mazungumzo na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo ofisini kwake jijini Dar es Salaaam.

Waziri Motegi, ambaye aliongoza Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Japani, alitaja maeneo kadhaa ambayo nchi yake ingependa kufanya uwekezaji ikiwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa umeme.

Aidha, wafanyabiashara walioambatana na Waziri Motegi, walimweleza Waziri Muhongo kuwa fursa za uwekezaji zilizopo nchini na zinazoendelea kubainika siku hadi siku hususan upatikanaji wa gesi asilia zimekuwa ni kivutio na kichocheo kikubwa kwao kutamani kuwekeza Tanzania.

Mbali na kuonesha nia ya kuwekeza hapa nchini, Wajapani wameonyesha utayari wa kuwasaidia Watanzania katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali zilizopo kwa kutoa mafunzo.

“Serikali yangu iko tayari kupokea wanafunzi kutoka Tanzania kwa ajili ya mafunzo katika fani ya masuala ya jotoardhi,” alisema Waziri Motegi. Hata hivyo alibainisha kuwa kwa sasa serikali yake inafanya maandalizi ya kuanza kupokea watanzania kwa mafunzo husika na kwamba endapo mambo yataenda sawa, huenda mafunzo yakaanza rasmi mapema mwakani.

Kwa upande wake, Waziri Muhongo aliishukuru Serikali ya Japani kwa utayari wa kuwapatia mafunzo Watanzania na kusisitiza kuwa hilo ni jambo la msingi kwa nchi kuweza kusimamia rasilimali zake kikamilifu.

“Serikali imedhamiria kuongeza wataalamu wazawa watakaoweza kusimamia rasilimali zetu vizuri pasipo kutegemea wataalamu kutoka nchi za nje,” alisema.

Aidha, Prof. Muhongo aliwahakikishia Wajapani kuwa Tanzania inazo fursa nyingi za uwekezaji na hivyo kuwakaribisha Wafanyabiashara hao kuja kuwekeza hususan katika miradi mbalimbali ya uzalishaji na usambazaji umeme kupitia vipaumbele vilivyoanishwa na serikali vya jototardhi, tungamotaka, gesi asilia, upepo na umemejua.


Imeandaliwa na:

Veronika H. Simba
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Selikarini
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print
«November 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
101112131415
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Tarehe 14 Novemba 2025.

Read more
16
Watumishi REA Wapongezwa

Watumishi REA Wapongezwa

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wapongezwa kwa kujituma na kufanya kazi kwa bidii hali iliyopelekea mafanikio makubwa ya Wakala huo ikiwamo kufikisha umeme katika Vijiji vyote vya Tanzania Bara.

Read more
171819
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemuapisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi pamoja na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Salome Wycliffe Makamba wakati wa Hafla ya kuwaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma Novemba 18, 2025

Read more
20212223
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top