Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Kilosa Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 915

Kilosa Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwafikishia mradi unaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wa kusambaza majiko yaliyoboreshwa maarufu kama majiko banifu kwa bei ya ruzuku ya shilingi 14,700 kwa kila jiko.

Wametoa shukrani hizo Agosti 6, 2025 wakati wa uzinduzi wa mradi shilingi 9,400,799,626.7 wa kusambaza majiko banifu ambayo yatasambazwa kote nchini kwa bei ya ruzuku uliyofanyikia eneo la Stendi wilayani humo ambapo Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaka Hamdu akiwa mgeni rasmi.

“Rais Samia ni mkombozi wetu, sisi wajasiriamali ametusaidia sana, kwanza alituletea majiko ya gesi kwa bei ya ruzuku na sasa tumepokea majiko haya banifu ambayo nayo yanakwenda kuwa msaada mkubwa kwa shughuli zetu za kila siku,” alisema Daines Samwel ambaye ni mjasiriamali la Stendi.

Naye Aisha Swai, mkazi wa Uhindini wilayani humo alisema majiko haya yanakwenda kupunguza gharama za maisha kwani hapo awali alikuwa akitumia zaidi ya shilingi 20,000 kununua mkaa kwaajili ya shughuli zake siku za mama lishe na kwamba kutokana na sifa ya majiko hayo ya kutumia mkaa mchache itamsaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli zake.

Akizindua mradi, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Shaka Hamdu alisema Wilaya ya Kilosa ni mnufaika mkubwa wa miradi inayosimamiwa na REA na aliipongeza kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia maono na maelekezo ya Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo ya usambazaji wa umeme na usambazaji wa nishati safi ya kupikia.

“Kwa hapa Kilosa, tunashukuru sana, vijiji vyote vimefikishiwa umeme na kazi inaendelea ya kufikisha umeme kwenye vitongoji; leo hii tupo hapa kuzindua mradi mkubwa wa zaidi ya shilingi bilioni tisa wa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku,” alisema Hamdu.

Alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia mradi huo ambao alisema ni suluhu ya uharibifu wa misitu inayoizunguka wilaya hiyo lakini pia ni mkombozi wa afya za wananchi hao ambao wamekuwa kwa kiwango kikubwa wakikata miti kwa ajili ya kuni za kupikia.

“Ndani ya wilaya ya Kilosa unaweza kusema kwa 100% wananchi wamekuwa wakitumia nishati isiyosalama, nishati ambayo siyo sahihi; tuliona njia nyepesi ni kutumia kuni lakini kumbe mambo yamebadilika misitu yetu inapaswa kubaki salama na afya zetu pia kutoathirika tena na moshi wa kuni,” alisisitiza Hamdu.

Akizungumzia mradi kwa ujumla wake, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alisema kuwa REA imejipanga kikamilifu kuhakikisha lengo lililomo katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia linafikiwa.

“Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imetambua changamoto wanayopata wananchi wake na ndio sababu imeweka ruzuku kubwa ili kuwafikia wananchi wengi Zaidi. Miti inakatwa kwa wingi, akina mama na watoto wanapata madhara kiafya na ili kuondokana na madhara haya tumejuka na majiko banifu nchi nzima na kwa kuanzia kwa hapa Morogoro kila wilaya itafikishiwa majiko 1,195,” alifafanua Mha. Advera.

Alibainisha kuwa kampuni saba zimeshinda zabuni za kusambaza majiko banifu katika mikoa mbalimbali kote nchini na kwamba kila mwananchi mwenye kuhitaji jiko banifu kupitia mradi huo anapaswa kuwa na kitambulisho cha Taifa ili kuiwezesha Serikali kutunza kumbukumbu na kupata takwimu halisi ya utekelezaji wa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia.

Mhadisi Advera alibainisha kuwa mradi huo wa majiko banifu unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali na Jumla ya majiko 200,000 yatasambazwa nchi nzima.

Alisema REA itaendelea kutekeleza miradi ya Nishati Safi ya kupikia nchi nzima na kwa kutumia vyanzo na teknojia mbalimbali ili kuhakikisha watanzania wengi wananufaika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top