Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Kilosa Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 676

Kilosa Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwafikishia mradi unaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wa kusambaza majiko yaliyoboreshwa maarufu kama majiko banifu kwa bei ya ruzuku ya shilingi 14,700 kwa kila jiko.

Wametoa shukrani hizo Agosti 6, 2025 wakati wa uzinduzi wa mradi shilingi 9,400,799,626.7 wa kusambaza majiko banifu ambayo yatasambazwa kote nchini kwa bei ya ruzuku uliyofanyikia eneo la Stendi wilayani humo ambapo Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaka Hamdu akiwa mgeni rasmi.

“Rais Samia ni mkombozi wetu, sisi wajasiriamali ametusaidia sana, kwanza alituletea majiko ya gesi kwa bei ya ruzuku na sasa tumepokea majiko haya banifu ambayo nayo yanakwenda kuwa msaada mkubwa kwa shughuli zetu za kila siku,” alisema Daines Samwel ambaye ni mjasiriamali la Stendi.

Naye Aisha Swai, mkazi wa Uhindini wilayani humo alisema majiko haya yanakwenda kupunguza gharama za maisha kwani hapo awali alikuwa akitumia zaidi ya shilingi 20,000 kununua mkaa kwaajili ya shughuli zake siku za mama lishe na kwamba kutokana na sifa ya majiko hayo ya kutumia mkaa mchache itamsaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli zake.

Akizindua mradi, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Shaka Hamdu alisema Wilaya ya Kilosa ni mnufaika mkubwa wa miradi inayosimamiwa na REA na aliipongeza kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia maono na maelekezo ya Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo ya usambazaji wa umeme na usambazaji wa nishati safi ya kupikia.

“Kwa hapa Kilosa, tunashukuru sana, vijiji vyote vimefikishiwa umeme na kazi inaendelea ya kufikisha umeme kwenye vitongoji; leo hii tupo hapa kuzindua mradi mkubwa wa zaidi ya shilingi bilioni tisa wa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku,” alisema Hamdu.

Alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia mradi huo ambao alisema ni suluhu ya uharibifu wa misitu inayoizunguka wilaya hiyo lakini pia ni mkombozi wa afya za wananchi hao ambao wamekuwa kwa kiwango kikubwa wakikata miti kwa ajili ya kuni za kupikia.

“Ndani ya wilaya ya Kilosa unaweza kusema kwa 100% wananchi wamekuwa wakitumia nishati isiyosalama, nishati ambayo siyo sahihi; tuliona njia nyepesi ni kutumia kuni lakini kumbe mambo yamebadilika misitu yetu inapaswa kubaki salama na afya zetu pia kutoathirika tena na moshi wa kuni,” alisisitiza Hamdu.

Akizungumzia mradi kwa ujumla wake, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alisema kuwa REA imejipanga kikamilifu kuhakikisha lengo lililomo katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia linafikiwa.

“Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imetambua changamoto wanayopata wananchi wake na ndio sababu imeweka ruzuku kubwa ili kuwafikia wananchi wengi Zaidi. Miti inakatwa kwa wingi, akina mama na watoto wanapata madhara kiafya na ili kuondokana na madhara haya tumejuka na majiko banifu nchi nzima na kwa kuanzia kwa hapa Morogoro kila wilaya itafikishiwa majiko 1,195,” alifafanua Mha. Advera.

Alibainisha kuwa kampuni saba zimeshinda zabuni za kusambaza majiko banifu katika mikoa mbalimbali kote nchini na kwamba kila mwananchi mwenye kuhitaji jiko banifu kupitia mradi huo anapaswa kuwa na kitambulisho cha Taifa ili kuiwezesha Serikali kutunza kumbukumbu na kupata takwimu halisi ya utekelezaji wa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia.

Mhadisi Advera alibainisha kuwa mradi huo wa majiko banifu unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali na Jumla ya majiko 200,000 yatasambazwa nchi nzima.

Alisema REA itaendelea kutekeleza miradi ya Nishati Safi ya kupikia nchi nzima na kwa kutumia vyanzo na teknojia mbalimbali ili kuhakikisha watanzania wengi wananufaika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top