Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Awafuta Machozi ya Kuni Akina Mama Nchini
Frank A. Mugogo 51

Rais Samia Awafuta Machozi ya Kuni Akina Mama Nchini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa shilingi 9,400,799,626.7 wa kusambaza majiko yaliyoboreshwa maarufu kama majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku ya asilimia 80 hadi 85 kote nchini.

Hayo yamesemwa Agosti 4, 2025 na mwakilishi wa REA Mkoani Morogoro, Mhandisi Cecilia Msangi wakati akimtambulisha Mtoa huduma aliyeshinda zabuni ya kusambaza majiko hayo Mkoani humo, kampuni ya Burn Manufacturing Tanzania Ltd katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

"Wakala unatekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia miradi mbalimbali ikiwemo huu wa kusambaza majiko banifu ambao rasmi leo hii tupo hapa kuutambulisha kwa wananchi wa Morogoro," alisema Mha. Msangi.

Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kampeni hiyo ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo alisema kwa jitihada zake binafsi hatua mbalimbali zimechukuliwa hususan za kuwanusuru akina mama kutokana na madhara ya moshi wa kuni sambamba na uhifadhi wa mazingira.

Alisema Rais Samia alitoa maelekezo mahususi ya kuhakikisha wananchi wanawezeshwa ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kupikia ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao umeelekeza ifikapo Mwaka 2034; 80% ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Akizungumza juu ya utekelezaji wa mradi kwa Mkoa wa Morogoro, Mha. Msangi alisema jumla ya majiko banifu 8,366 yatatolewa kwa bei ya ruzuku ya shilingi 14,694 kwa kila jiko.

"Kwa bei ya kawaida kabla ruzuku jiko hilo lilikuwa likiuzwa shilingi 73,468.36 na sasa baada ya kupokea kwa ruzuku ya 80% jiko hilo litauzwa kwa shilingi 14,694 tu," alibainisha Mhandisi Msangi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mussa Mussa alipongeza jitihada za REA na alisema kuwa manufaa yatakayopatikana kutokana na mradi huo ni makubwa kuliko hata inavyotarajiwa.

"Haya majiko namna yalivyosanifiwa yanatumia mkaa kidogo na pia yanatunza joto kwa muda mrefu, hivyo inakwenda kumpunguzia mwananchi gharama za mkaa na kumuokolea muda," alisisitiza Katibu Tawala, Musa.

Aidha, Meneja wa Kampuni ya Burn Manufacturing Tanzania Ltd, John Mtui alisema kampuni yao imeshinda zabuni ya kusambaza majiko banifu 39,286 katika Mikoa ya Morogoro, Ruvuma, Kagera na Tabora ambayo ni sawa na shilingi 2,309,022,392.77.
"Hapa Morogoro tutasambaza jumla ya majiko 8,366 katika Wilaya za Gairo, Kilombero, Kilosa, Malinyi, Morogoro Vijijini, Ulanga na Mvomero ambapo kila wilaya itapata majiko 1,196," alisema Mtui.

REA inatekeleza miradi mbalimbali nchini kwa kuwezesha na kuelimisha wananchi kuachana na matumizi ya nishati zisizo safi na salama kwa afya zao na mazingira kwa ujumla.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top