Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi
Mohamed Saif 253

Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Kusambazwa wilaya zote za Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruzuku ya shilingi 7,500 yanayosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kulinda afya, kuokoa misitu na kuhifadhi mazingira.

Ametoa rai hiyo Desemba 18, 2025 Mkoani Katavi wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusambaza majiko banifu ya ruzuku yapatayo 3,126 mkoani humo unaotekelezwa na Kampuni ya Tango Energy Ltd ya Jijini Dar es Salaam unaoratibiwa na kusimamiwa na REA wenye thamani ya shilingi milioni 156.3 ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034).

“Nitoe wito kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi, majiko haya ni kwa ajili yenu na yameuzwa kwa bei ya ruzuku kwa maana ya kwamba Serikali imelipia zaidi ya shilingi 50,000 lakini mwananchi analipia shilingi 7,500 pekee, naomba mchangamkie fursa hii,” amesisitiza Mhe, Mrindoko.

Mhe. Mrindoko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amejielekeza katika kuhakikisha kwamba wananchi wote wanatumia nishati safi ya kupikia.

Alisisitiza wananchi wa Katavi kuhakikisha maono na maelekezo ya Rais ya kuendelea kutunza misitu yanatekelezwa na kwamba kupitia mradi wa kusambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku utawezesha uhifadhi wa misitu.

“Tunamshukuru Rais na tunamhakikishia kwamba afua zote zinazohusiana na utunzaji wa mazingira, utunzaji wa misitu kwa kusaidiana na Wakuu wa Wilaya na watendaji tutahakikisha jambo hili linafanikiwa kikamilifu ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa,” alisema Mhe. Mrindoko.

Akitambulisha mradi, Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka REA, Dkt. Joseph Sambali alisema majiko hayo yatauzwa kwa shilingi 7,500 badala ya shilingi 59,000 kwakuwa Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya 85% sambamba na kuondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika majiko hayo ili kumpa unafuu mwananchi.

“Kabla ya ruzuku jiko moja lilikuwa likiuzwa kwa shilingi 59,000 na baada ya Serikali kuweka ruzuku likauzwa kwa shilingi 8,850 lakini sasa baada pia ya kuondoa kodi ya VAT jiko moja hapa Katavi litauzwa kwa shilingi 7,500 pekee," alibainisha Dkt. Sambali.

Alisema katika kila Wilaya majiko banifu 1,042 yatasambazwa ambayo jumla yake ni majiko 3,126 ambapo alizitaja wilaya hizo kuwa ni Mpanda, Mlele na Tanganyika.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tango Energy Ltd, Musa Msofe alisema wamejipanga ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwamba majiko hayo yatauzwa kwa bei ya ruzuku kwa mwananchi mwenye kitambulisho cha Taifa (NIDA) na kwamba majiko hayo yana udhamini (warranty) wa mwaka mmoja.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top