Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA
Aodax K. Nshala 2949

MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA

Tarehe 25 Septemba 2021, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu alitoa taarifa kwa umma ikieleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemteua Mhandisi Hassan Seif Said kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa uteuzi wa Mhandisi Said, ambaye awali alikuwa Meneja wa Kanda Mwandamizi wa Kanda ya Mashariki TANESCO, umeanza tarehe 23 Septemba, 2021.

REA inatoa pongezi za dhati kwa Mhandisi Said kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kuiongoza REA. Tunaahidi kumpatia ushirikiano katika kazi yake ili azma ya Serikali ya kuwapatia wananchi wote nishati bora na ya uhakika iendelee kutekelezwa.

Aidha, tunamshukuru Mtangulizi wake, Mhandisi Amos William Maganga, kwa utumishi wake katika kuiongoza sekta husika katika kipindi chote alichotumikia kama Mkurugenzi Mkuu wa REA.

Karibu sana Mhandisi Hassan Seif Said na asante kwa utumishi wako Mhandisi Amos William Maganga. Kazi iendelee…

Share

Print

Documents to download

«May 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
27282930123
45678
Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Read more
910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top