Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA
Aodax K. Nshala 2213

MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA

Tarehe 25 Septemba 2021, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu alitoa taarifa kwa umma ikieleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemteua Mhandisi Hassan Seif Said kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa uteuzi wa Mhandisi Said, ambaye awali alikuwa Meneja wa Kanda Mwandamizi wa Kanda ya Mashariki TANESCO, umeanza tarehe 23 Septemba, 2021.

REA inatoa pongezi za dhati kwa Mhandisi Said kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kuiongoza REA. Tunaahidi kumpatia ushirikiano katika kazi yake ili azma ya Serikali ya kuwapatia wananchi wote nishati bora na ya uhakika iendelee kutekelezwa.

Aidha, tunamshukuru Mtangulizi wake, Mhandisi Amos William Maganga, kwa utumishi wake katika kuiongoza sekta husika katika kipindi chote alichotumikia kama Mkurugenzi Mkuu wa REA.

Karibu sana Mhandisi Hassan Seif Said na asante kwa utumishi wako Mhandisi Amos William Maganga. Kazi iendelee…

Share

Print

Documents to download

«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top