Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA
Aodax K. Nshala 2297

MHANDISI HASSAN SEIF SAIDY ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA REA

Tarehe 25 Septemba 2021, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu alitoa taarifa kwa umma ikieleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemteua Mhandisi Hassan Seif Said kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa uteuzi wa Mhandisi Said, ambaye awali alikuwa Meneja wa Kanda Mwandamizi wa Kanda ya Mashariki TANESCO, umeanza tarehe 23 Septemba, 2021.

REA inatoa pongezi za dhati kwa Mhandisi Said kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kuiongoza REA. Tunaahidi kumpatia ushirikiano katika kazi yake ili azma ya Serikali ya kuwapatia wananchi wote nishati bora na ya uhakika iendelee kutekelezwa.

Aidha, tunamshukuru Mtangulizi wake, Mhandisi Amos William Maganga, kwa utumishi wake katika kuiongoza sekta husika katika kipindi chote alichotumikia kama Mkurugenzi Mkuu wa REA.

Karibu sana Mhandisi Hassan Seif Said na asante kwa utumishi wako Mhandisi Amos William Maganga. Kazi iendelee…

Share

Print

Documents to download

«May 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2829301234
567891011
12131415
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Read more
16
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Read more
1718
19
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Read more
202122
Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 20 wa kusambaza umeme katika vitongoji 180 utakaonufaisha zaidi ya Kaya 5,940 Mkoani Tanga.

Read more
232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top