Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara
Mohamed Saif 156

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme REA, Mha. Deogratius Nagu ametoa maelekezo hayo Januari 29, 2026 kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi katika Wilaya za Nanyumbu, Newala, Tandahimba na Masasi Mkoani Mtwara.

"Kasi ya utekelezaji wa mradi hairidhishi, jitahidini kuongeza kasi, tafuteni watoa huduma wa vifaa wengi ili ikitokea mmoja kachelewa mnachukua kwa mwingine," alielekeza Mha. Nagu.

Alisema kutegemea mtoa huduma mmoja mmoja kwa kila kifaa ni jambo la hatari kwani ikitokea amechelewa kugikisha vifaa site, kazi zinasimama na kuchelewesha kukamilika kwa mradi na aliwasisitiza kufanya kazi na Watoa huduma wanaotambuliwa na walio katika kanzidata za TANESCO ili kupata vifaa vyenye ubora unaokubalika.

Mha. Nagu alisema Mkandarasi wa Mradi Kusambaza Umeme atakayefanya vizuri anayo nafasi kubwa ya kupata kazi ya kutekeleza mradi mwingine.

"Mnapaswa kuwasimamia kwa karibu hawa wanaowasambazia vifaa mathalan huyu anayewauzia transfoma hakikisheni mnaweka mtu wenu maalum kiwandani kwa ajili ya kufuatilia kukamilika kwa taratibu za kusafirisha transfoma hizo kuja site," alielekeza Mha. Nagu.

Kwa upande wake Meneja Mradi kutoka Kampuni ya Nothern Engineering, Mha. Christopher Masasi alikiri kuwepo kwa changamoto ya kucheleweshewa vifaa kutoka kwa watoa huduma na aliahidi kuongeza idadi ya watoa huduma watakosambaza vifaa kwa ajili ya mradi.

"Ni kweli hatuna changamoto zaidi ya hii ya kucheleweshewa vifaa na watoa huduma, tumepokea maelekezo na tunaahidi kuongeza kasi na leo hii tumepokea shehena ya vifaa hivyo kasi itaongezeka," alisema Mha. Masasi.

Aidha, kwa mujibu wa Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoani Mtwara, Mha. Daniel Mwandupe amesema Mkandarasi Nothern Engineering Works Limited anatekeleza mradi wenye thamani ya shilingi 16,717,407,821.65 utakaonufaisha Kaya 4,950.

Mha. Mwandupe amesema hadi sasa Mkandarasi amewasha vitongoji 40 na kuunga wateja 458 na anatarajiwa kukamilisha mradi ifikapo Agosti mwaka huu.

Share

Print
«March 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2324252627281
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
303112345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top