Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi
Frank A. Mugogo 753

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
 
Wito huo umetolewa leo Agosti 18, 2025 Mkoani Rukwa na Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Florian Haule wakati wa ugawaji wa mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Rukwa unaotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
 
Akiwa ameambatana na Mjumbe wa Bodi hiyo, Stephen Mwakifwamba, Haule amewataka pia maafisa pamoja na askari wa jeshi hilo kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia kwa jamii inayowazunguka.
 
"Ni ukweli usiopingika kwamba Jeshi la Magereza hapo nyuma walikuwa ni wakala wakubwa wa uharibifu wa mazingira kwa kutumia kuni na mkaa kwa ajili ya kuandaa chakula cha wafungwa magerezani, hali iliyopelekea uharibifu wa mazingira hasa uoto wa asili. Lakini kwa sasa magereza yote yanatumia nishati safi ya kupikia.
 
Matumizi ya nishati safi ya kupikia yanakwenda kuokoa mazingira yetu na hivyo kupunguza madhara ya kiuchumi pamoja na kijamii ambayo yanatokana na mabadiliko ya tabia nchi. Niendelee kuwahamasisha mkawe mabalozi wazuri wa nishati safi ya kupikia ili tuendelee kulinda mazingira yetu," amesema Haule.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Vendeline Tesha amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha magereza yote katika Mkoa huo kufungwa mifumo ya nishati safi ya kupikia na kuwezesha pia askari wa jeshi hilo kupata majiko ya gesi na kuongeza kuwa kitendo hicho kitaenda kuongeza morali ya kazi kwa watumishi hao.
 
Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili maono ya Mhe. Rais pamoja na malengo ya Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao umebainisha kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia yanafikiwa.
 
Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Afisa kutoka REA, Mhandisi Francis Manyama amesema kuwa kwa Mkoa wa Rukwa, jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 297 yamepangwa kugaiwa kwa watumishi wa jeshi la magereza katika Mkoa wa Rukwa.
 
Septemba 13, 2024, REA iliingia makubaliano ya utekelezwaji wa mradi wenye gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 35 na Jeshi la Magereza wa kuwezesha kutoa ruzuku kwa ajili ya kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa magereza yote ya Tanzania Bara.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top