Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Imefanya Kazi Kubwa ya Kufikisha Huduma za Nishati Vijijini
Mohamed Saif 53

REA Imefanya Kazi Kubwa ya Kufikisha Huduma za Nishati Vijijini

Waziri Ndejembi asisitiza ubunifu katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kufikisha umeme kwenye vijiji na maeneo ya pembezoni mwa miji iliyopelekea kukuza shughuli za kiuchumi katika maeneo hayo.

Pongezi hizo zimetolewa leo Novemba 28, 2025 wakati Mhe. Ndejembi alipokutana na kuzungumza na Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya REA kuhusu utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini na vitongojini pamoja na utekelezaji wa Mkakati wa nishati safi ya kupikia katika kikao kilichofanyika Ofisi za Makao Makuu ya REA jijini Dodoma.

"REA imefanya kazi kubwa na nzuri sana hapa nchini hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. Kipekee nachukua fursa hii kuipongeza sana Bodi ya REA, Menejimenti na Wafanyakazi kwa ujumla kwa kufanya kazi kubwa ya kupeleka umeme katika vijijini vyote nchini, " Amesema Mhe. Ndejembi.

Mhe. Ndejembi ameongeza kuwa, umeme vijijini haukuwa kama ilivyo leo na kuna watu walidhani kwamba kufikisha umeme kwenye vijiji vyote ni hadithi na haitowezekana lakini sasa vijiji vyote vimesambaziwa umeme hapa nchini na REA imefanya kazi kubwa.

Aidha, Mhe. Ndejembi ameipogeza REA kwa kushirikiana kwa karibu na wadau wengine wakiwemo TANESCO ambao kwa kiasi kikubwa wameshiriki katika kufikisha mafanikio ya Wakala katika utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.

Naye, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Matarajio amesema kuwa, REA ni taasisi inayohakikisha kuwa Watanzania waliopo maeneo ya vijijini wanapata nishati safi na bora ya umeme ili waweze kufanya shughuli zao kwa tija kupitia nishati hiyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Meja Jenerali Mstaafu, Mhe. Balozi Jacob Kingu amesema kuwa REB itatoa ushirikiano wa kutosha kwa Waziri Ndejembi katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za miradi ya umeme vijijini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amesema kuwa vijiji vyote 12,318 tayari vimefikishiwa huduma ya umeme.

"Ufikishaji umeme kwenye vitongoji hadi sasa ni 39,003 kati ya 64,359 sawa na asilimia 61, vitongoji 2,562 vipo kwenye miradi inayoendelea (Densification 2A, HEP I, HEP IIA, HEP Lindi), " Amesema Mha. Saidy.

Halikadhalika mradi kusambaza umeme kwenye vitongoji (HEP 2B) wa vitongoji 9,000 utatekelezwa katika kila mkoa hapa nchini ambapo mradi utakuwa wa miaka mitatu na wateja wa awali wanatarajiwa kuwa 290,000.

Kuhusu nishati safi amesema REA inawezesha na kuhamasisha upatikanaji wa nishati safi kwa wananchi vijijini na pembezoni mwa miji, miradi hiyo inahusisha gesi asilia, LPG, majiko banifu na mifumo ya nishati safi katika taasisi.

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
17
REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

Read more
1819
Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruzuku ya shilingi 7,500 yanayosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kulinda afya, kuokoa misitu na kuhifadhi mazingira.

Read more
2021
REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top