Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini
Frank A. Mugogo 124

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma Novemba 25, 2025 wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba na Menejimenti ya REA kilicholenga kujadili utekelezaji wa miradi inayosimamiwa na REA.

Mhe. Salome amesema Serikali kupitia REA inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kufikisha umeme katika vitongoji 9,000 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa wananchi.

“Serikali inatekeleza mipango madhubuti itakayoleta matokeo ya haraka kwa wananchi wake kupitia Sekta ya Nishati. Ndani ya siku mia moja kupitia REA tunatekeleza ahadi ya Mhe. Rais ya kufikisha umeme kwa wananchi,” amesema Mhe. Salome.

Akizungumzia eneo la Nishati Safi ya Kupikia, Mhe. Salome amesema REA itajenga mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia kwa zaidi ya taasisi 50 ili kuziwezesha kuhama kutoka kwenye matumizi ya nishati isiyo safi na salama.

“Ndani ya siku mia moja wananchi watashuhudia mabadiliko kwani tunakwenda kufunga mifumo ya Nishati safi ya Kupikia kwenye taasisi na tayari matangazo yametolewa, taasisi ziendelee kuchangamkia,” alisema.

Ametoa wito kwa wananchi hususani vijana kuchangamkia fursa zilizopo kwenye mnyororo wa uboreshaji na usambazaji wa teknolojia za nishati safi ya kupikia zinazotolewa na Serikali kupitia REA.

Aidha, ameelekeza wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kusambaza umeme vitongojini kuhakikisha wanakwenda na kasi ya Serikali kwa kukamilisha miradi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa hasa ikizingatiwa kuwa fedha nyingi inatumika kutekeleza miradi hiyo na kwamba Serikali haitomvumilia mkandarasi mzembe.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy alibainisha hatua mbalimbali zinazochukuliwa na hali ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati safi maeneo ya vijijini.

Mha. Saidy alitoa wito kwa wananchi waishio maeneo ya vijijini kuchangamkia fursa ya kujiunganisha na huduma ya umeme na kwamba Serikali inaanza kutoa ruzuku kwa wananchi kwa ajili ya kuweka mifumo ya kutandaza nyaya ndani ya nyumba (wiring).

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«January 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2930311234
5678910
Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kata za Wendele na Mwendakulima Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadilisha maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
11
12131415161718
19202122232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top