Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe
Frank A. Mugogo 241

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Mkuu wa mkoa wa Songwe, Mhe. Daniel Chongolo amewapongeza REA pamoja na msambazaji, kampuni ya Oryx Gas kwa kuanza kugawa mitungi hiyo katika muda muhafaka na kutoa wito kwa REA na wasambazaji kuendelea kutoa elimu kuhusu usalama wa gesi; na faida ya matumizi ya nishati safi na salama kiafya na namna zinvyochangia katika utunzaji na uhifadhi mazingira.

“Mpango huu wa kusambaza mitungi ya gesi ni mzuri na kama mnavyofahamu; Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mama Samia Suluhu Hassan ni Mhamasishaji namba moja wa nishati safi siyo tu barani Afrika bali Duniani kote, kwa ujumla na sisi tunaoishi mikoa ya pembezoni, ndiyo waathirika wakubwa wa changamoto zinazotokana na matumizi ya nishati zisizo safi.” 

"Naipongeza REA kwa kuanza kutekeleza Mradi huu, nawapongeza pia Oryx Gas kwa kuwa sehemu ya ajenda ya kusambaza nishati safi kwa Watanzani. Huu ni uzalendo wa hali ya juu kwa Taifa letu” amesema Mhe. Chongolo. 

Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Nishati Safi mkoa wa Songwe kutoka REA; Bwana Vencha Maganga amesema, Serikali kupitia REA imetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya kusambaza nishati safi ikiwemo gesi (LPG) katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji na kuwaomba Wananchi wa mkoa wa Songwe kuchangamkia fursa ya kununua mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku ambayo ni shilingi 20,000 tu kwa mtungi wa gesi wa kilo sita (6) na fedha inayobaki, inalipwa na Serikali.

"Lengo letu ni kutoa elimu na kuwawezesha Wamama ambao ndiyo watumiaji wakubwa wa nishati chafu ili wapate nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati zisizo safi. Nawaomba Wananch wafike kwenye vituo vya kuuzia mitungi hiyo, wakiwa na Vitambulisho vya NIDA kwa ajili kununua mitungi hii pamoja na vifaa vyake kwa bei ya ruzuku ya shilingi (20,000/=) tofauti na ambavyo wangenunua kwa shilingi (40,000) na kuendelea hadi shilingi (60,000)”. Ameongeza Bwana Maganga.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi; Mhe. George Msyani amewapongeza Wananchi kufika kwenye kituo cha mauzo ili kununua mitungi hiyo ya gesi kwa bei ya ruzuku katika kitongoji cha Mlowo, wilayani Mbozi.

Wilaya zitakazonufaika na usambazaji wa mitungi hiyo ya gesi kwa mkoa wa Songwe ni pamoja Mbozi, Ileje, Momba na Songwe

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top