Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaendelea Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo
Frank A. Mugogo 163

REA Yaendelea Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea na jitihada mbalimbali za uelimishaji, uhamasishaji na usambazaji wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia katika Mikoa yote Tanzania Bara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa lengo la  kuhakikisha 80% ya Wananchi wanatumia Nishati Safi za Kupikia ifikapo Mwaka 2034.

Hayo yameelezwa Machi 7, 2025 Jijini Arusha na Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi REA, Mhandisi Emanuel Yesaya wakati wa Maonesho ya Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani 2025.

"Tunashiriki kutoa elimu, kuonyesha bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia na kuhamasisha wananchi hususan akina mama kutumia nishati safi ya kupikia ili kurahisisha maisha yao sambamba na kulinda afya zao," alisema Mhandisi Yesaya

Alisema REA imeandaa program mbalimbali zinazolenga kumrahisishia maisha mwanamke hasa ikizingatiwa kuwa mwanamke ndiye kinara wa jiko.

Alisema Serikali inatambua umuhimu wa kulinda afya za wananchi wake sambamba na kuhifadhi mazingira ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiriwa na matumizi ya Nishati chafu za kupikia zikiwemo kuni na mkaa na sasa mwelekeo ni kujikita katika matumizi ya Nishati Safi za Kupikia ambazo Serikali inafanya kila njia zifike kwa kila mwananchi kwa gharama anayoweza kumudu.

"Hii ni fursa adhim ambayo imetolewa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye kinara wa Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi wake, tunatoa rai kwa Watanzania kuchangamkia fursa hii," alisema Mhandisi Yesaya.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa REA, Bi Martha Chassama alitoa wito kwa wanawake kutembelea banda la Wizara ya Nishati ili kujifunza kwa undani umuhimu wa kutumia Nishati Safi ya Kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top