Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA
Frank A. Mugogo 400

Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hayo yameelezwa Mei 27,2025 katika Banda la REA Jijini Dar es Salaam na Mhandisi Miradi kutoka REA, Raya Majallah kwa Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti.

"Tunaendelea na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia nyenzo mbalimbali ili kuhakikisha tunafanikiwa kufikisha lengo la 80%," alisema Mha. Raya.

Pedetti alipongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na REA na alisisitiza REA iendelee na utoaji wa elimu ili wananchi watambue umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia.

Katika maadhimisho hayo REA kwa kushirikiana na wadau wake imepata fursa ya kuonesha teknolojia za bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, sambamba na kushiriki kikamilifu mijadala mbalimbali kuhusu nafasi ya nishati jadidifu katika kufikia lengo la taifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu. yamefunguliwa rasmi na Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti akimwakilisha Balozi wa Umoja wa Ulaya.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top