Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA
Frank A. Mugogo 360

Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hayo yameelezwa Mei 27,2025 katika Banda la REA Jijini Dar es Salaam na Mhandisi Miradi kutoka REA, Raya Majallah kwa Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti.

"Tunaendelea na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia nyenzo mbalimbali ili kuhakikisha tunafanikiwa kufikisha lengo la 80%," alisema Mha. Raya.

Pedetti alipongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na REA na alisisitiza REA iendelee na utoaji wa elimu ili wananchi watambue umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia.

Katika maadhimisho hayo REA kwa kushirikiana na wadau wake imepata fursa ya kuonesha teknolojia za bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, sambamba na kushiriki kikamilifu mijadala mbalimbali kuhusu nafasi ya nishati jadidifu katika kufikia lengo la taifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu. yamefunguliwa rasmi na Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti akimwakilisha Balozi wa Umoja wa Ulaya.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
1718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top