Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA
Frank A. Mugogo 497

Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hayo yameelezwa Mei 27,2025 katika Banda la REA Jijini Dar es Salaam na Mhandisi Miradi kutoka REA, Raya Majallah kwa Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti.

"Tunaendelea na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia nyenzo mbalimbali ili kuhakikisha tunafanikiwa kufikisha lengo la 80%," alisema Mha. Raya.

Pedetti alipongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na REA na alisisitiza REA iendelee na utoaji wa elimu ili wananchi watambue umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia.

Katika maadhimisho hayo REA kwa kushirikiana na wadau wake imepata fursa ya kuonesha teknolojia za bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, sambamba na kushiriki kikamilifu mijadala mbalimbali kuhusu nafasi ya nishati jadidifu katika kufikia lengo la taifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu. yamefunguliwa rasmi na Mkuu wa Idara ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya, Max Pedetti akimwakilisha Balozi wa Umoja wa Ulaya.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top