Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Lesotho Wavutiwa na REA
Frank A. Mugogo 321

Lesotho Wavutiwa na REA

Serikali ya Lesotho imevutiwa na namna ambavyo Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijiji (REA) imepiga hatua katika suala zima la usambazaji wa nishati safi maeneo ya vijijini.

Hayo yamebainishwa Mei 27, 2025 Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Nchini Lesotho, Tankiso Phapano akiwa ameambata na ujumbe wa wataalam katika Sekta ya Nishati nchini humo.

"Tumefuatilia kwa karibu katika suala la Nishati, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua na zilizofanikiwa kwa upana wake na tupo hapa leo hii kubadilishana uzoefu na kujifunza siri hii ya mafanikio iliyowafikisha hapa," alisema Phapano.

Alipongeza jitihada binafsi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika suala la uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wake.

Akizungumzia hali ya usambazaji wa nishati maeneo ya vijijini nchini Lesotho, Meneja Kitengo cha Umeme Vijijini (REU), Leloko Mokhutsoane alisema kwa sasa nchini humo, suala la usambazaji wa umeme maeneo ya vijijini linasimamiwa na kitengo kilicho ndani ya Shirika la Umeme la Lethoso (LEC).

Alisema kutokana na kusuasua kwa ufanisi wa kitengo hicho pamoja na mahitaji ya nishati safi ya kupikia hisusan maeneo ya vijijini nchi hiyo inakwenda kuanzisha Wakala wa Nishati Vijijini.

"Hiki ni kitengo tu tena kinahusika na umeme peke yake na sio nishati kwa upana wake; kwa sasa nasi tunataka kuwa na Wakala wa Nishati Vijijini kama ilivyo hapa Tanzania ili suala la nishati safi nalo liingie na tusijifungie kwenye umeme tu," alisema Mokhutsoane.

Akizungumzia uendeshaji wa shughuli za Wakala hapa nchini kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Hassan Saidy, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi Jones Olotu alieleza historia ya wakala hadi kufika sasa.

Mhandisi Olotu aliueleza ujumbe huo namna ambavyo REA ilianzishwa, mafanikio iliyopata hadi sasa sambamba na mipango inayoendelea kutekelezwa.

"REA Tanzania ilianzishwa rasmi mwaka 2007 na wakati huo vijiji 506 pekee vilikuwa vimefikiwa na umeme kati ya vijiji 12,318," alifafanua Mha. Olotu.

Aidha, Mha. Olotu alieleza kuwa Tanzania Bara ina jumla ya vitongoji 64,359 ambapo hadi sasa vitongoji 33,657 sawa na asilimia 52.3 tayari vimeshafikishiwa umeme.

Aliongeza kuwa, upelekaji wa umeme katika vitongoji 30,702 unaendelea ambapo vitongoji 7,736 vipo katika miradi inayoendelea na vitongoji 9,000 REA ipo katika hatua ya ununuzi wa wakandarasi ambao inatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2025.

Aliueleza ujumbe huo kuwa hadi kufikia mwaka huu 2025 vijiji vyote 12,318 vimefikishiwa nishati ya umeme na sasa kazi inayoendelea ni kufikisha umeme katika vitongoji.

Ujumbe huo ulipata wasaa wa kujadiliana na wataalam kutoka REA masuala mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za Wakala.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top