Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Lesotho Wavutiwa na REA
Frank A. Mugogo 49

Lesotho Wavutiwa na REA

Serikali ya Lesotho imevutiwa na namna ambavyo Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijiji (REA) imepiga hatua katika suala zima la usambazaji wa nishati safi maeneo ya vijijini.

Hayo yamebainishwa Mei 27, 2025 Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Nchini Lesotho, Tankiso Phapano akiwa ameambata na ujumbe wa wataalam katika Sekta ya Nishati nchini humo.

"Tumefuatilia kwa karibu katika suala la Nishati, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua na zilizofanikiwa kwa upana wake na tupo hapa leo hii kubadilishana uzoefu na kujifunza siri hii ya mafanikio iliyowafikisha hapa," alisema Phapano.

Alipongeza jitihada binafsi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika suala la uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wake.

Akizungumzia hali ya usambazaji wa nishati maeneo ya vijijini nchini Lesotho, Meneja Kitengo cha Umeme Vijijini (REU), Leloko Mokhutsoane alisema kwa sasa nchini humo, suala la usambazaji wa umeme maeneo ya vijijini linasimamiwa na kitengo kilicho ndani ya Shirika la Umeme la Lethoso (LEC).

Alisema kutokana na kusuasua kwa ufanisi wa kitengo hicho pamoja na mahitaji ya nishati safi ya kupikia hisusan maeneo ya vijijini nchi hiyo inakwenda kuanzisha Wakala wa Nishati Vijijini.

"Hiki ni kitengo tu tena kinahusika na umeme peke yake na sio nishati kwa upana wake; kwa sasa nasi tunataka kuwa na Wakala wa Nishati Vijijini kama ilivyo hapa Tanzania ili suala la nishati safi nalo liingie na tusijifungie kwenye umeme tu," alisema Mokhutsoane.

Akizungumzia uendeshaji wa shughuli za Wakala hapa nchini kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Hassan Saidy, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi Jones Olotu alieleza historia ya wakala hadi kufika sasa.

Mhandisi Olotu aliueleza ujumbe huo namna ambavyo REA ilianzishwa, mafanikio iliyopata hadi sasa sambamba na mipango inayoendelea kutekelezwa.

"REA Tanzania ilianzishwa rasmi mwaka 2007 na wakati huo vijiji 506 pekee vilikuwa vimefikiwa na umeme kati ya vijiji 12,318," alifafanua Mha. Olotu.

Aidha, Mha. Olotu alieleza kuwa Tanzania Bara ina jumla ya vitongoji 64,359 ambapo hadi sasa vitongoji 33,657 sawa na asilimia 52.3 tayari vimeshafikishiwa umeme.

Aliongeza kuwa, upelekaji wa umeme katika vitongoji 30,702 unaendelea ambapo vitongoji 7,736 vipo katika miradi inayoendelea na vitongoji 9,000 REA ipo katika hatua ya ununuzi wa wakandarasi ambao inatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2025.

Aliueleza ujumbe huo kuwa hadi kufikia mwaka huu 2025 vijiji vyote 12,318 vimefikishiwa nishati ya umeme na sasa kazi inayoendelea ni kufikisha umeme katika vitongoji.

Ujumbe huo ulipata wasaa wa kujadiliana na wataalam kutoka REA masuala mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za Wakala.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top