Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA
Mohamed Saif 169

Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Shughuli za kiuchumi na kijamii zimeimarika

Wananchi Kata za Wendele na Mwendakulima Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadilisha maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wametoa shukrani hizo kwa Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba kwa nyakati tofauti Januari 10, 2026 wakati wa hafla ya kuwasha umeme kwenye kitongoji cha Majengo Kata ya Wendele na Kitongoji cha Chapulwa Kata ya Mwendakulima.

"Ni neema kubwa kupata umeme, tunaishukuru Serikali kwa kutufikishia umeme, maisha yetu yanabadilika," alisema Mariam Manyesha Mkazi wa Kitongoji cha Majengo.

Mara baada ya kuwasha umeme, Naibu Waziri Mhe. Salome alizungumza na wananchi na kuwaeleza namna ambavyo Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi - CCM (2025-2030).

Mhe. Salome alibainisha kuwa Rais Samia ameelekeza ndani ya mwaka huu kaya 1,700,000 nchini wawe wameunganishwa na huduma ya umeme na kwamba tayari utekelezaji wa maelekezo hayo unaendelea. 

"Niwahakikishie tunaendelea kutekeleza maelekezo ya Rais, umeme ni kichocheo cha uchumi tumeshuhudia mabadiliko makubwa kwenye maeneo yaliyofikishiwa umeme na kipaumbele chetu ni kuwasha umeme," amesema Mhe. Salome.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mha. Jones Olotu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, alieleza namna ambavyo REA imejipanga kufikisha umeme kwenye vitongoji vyote nchini.

Alisema REA inaendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme vitongojini na kwamba hivi karibuni itasainiwa mikataba ya kusambaza umeme katika vitongoji 9009 kote nchini.

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
17181920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top