Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA
Mohamed Saif 83

Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Shughuli za kiuchumi na kijamii zimeimarika

Wananchi Kata za Wendele na Mwendakulima Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadilisha maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wametoa shukrani hizo kwa Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba kwa nyakati tofauti Januari 10, 2026 wakati wa hafla ya kuwasha umeme kwenye kitongoji cha Majengo Kata ya Wendele na Kitongoji cha Chapulwa Kata ya Mwendakulima.

"Ni neema kubwa kupata umeme, tunaishukuru Serikali kwa kutufikishia umeme, maisha yetu yanabadilika," alisema Mariam Manyesha Mkazi wa Kitongoji cha Majengo.

Mara baada ya kuwasha umeme, Naibu Waziri Mhe. Salome alizungumza na wananchi na kuwaeleza namna ambavyo Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi - CCM (2025-2030).

Mhe. Salome alibainisha kuwa Rais Samia ameelekeza ndani ya mwaka huu kaya 1,700,000 nchini wawe wameunganishwa na huduma ya umeme na kwamba tayari utekelezaji wa maelekezo hayo unaendelea. 

"Niwahakikishie tunaendelea kutekeleza maelekezo ya Rais, umeme ni kichocheo cha uchumi tumeshuhudia mabadiliko makubwa kwenye maeneo yaliyofikishiwa umeme na kipaumbele chetu ni kuwasha umeme," amesema Mhe. Salome.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mha. Jones Olotu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, alieleza namna ambavyo REA imejipanga kufikisha umeme kwenye vitongoji vyote nchini.

Alisema REA inaendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme vitongojini na kwamba hivi karibuni itasainiwa mikataba ya kusambaza umeme katika vitongoji 9009 kote nchini.

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top