Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wananchi Morogoro Wahimizwa Kufanya Wiring Kupokea Umeme
Iddy Mwema 122

Wananchi Morogoro Wahimizwa Kufanya Wiring Kupokea Umeme

Wananchi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro wamehimizwa kufanya maandalizi ya kupokea huduma ya umeme kwa kutandaza nyaya kwenye nyumba zao (wiring) ili kujitayarisha na miradi inayoendela ya umeme kwenye vitongoji.

 

Wito huo umetolewa leo Mei 19, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu wakati wa ziara ya kutembelea miradi ya kufikisha umeme inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Mkoa wa Morogoro.

 

Katika ziara hiyo, Mwenyekiti Kingu alitembelea Vijiji vya Ulundo pamoja na Mtego wa Simba ambako miradi ya REA ya kufikisha umeme kwenye vitongoji inaendelea kutekelezwa. Akiwa huko, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanafanya wiring mapema ili miundombinu ya umeme kwenye vitongoji itakapokamilika waweze kuunganisha umeme.

 

“Umeme kwa sasa ni hitaji la msingi. Unabadilisha maisha ya watu, unaongeza uzalishaji na kuboresha huduma muhimu za kijamii kama afya na elimu,” amesema Balozi Kingu huku akitoa wito pia kwa taasisi za serikali kama shule na vituo vya afya kuhakikisha wanavuta umeme kwenye taasisi zao ili kuendelea kuboresha huduma kwa jamii.

 

Balozi Kingu alieleza kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika kuboresha huduma za afya vijijini kwa kujenga vituo vya afya na zahanati pamoja na kupeleka vifaa tiba vya kisasa, lakini changamoto ya ukosefu wa umeme imekuwa ikikwamisha utoaji wa huduma bora.

 

Awalia, akitoa taarifa kuhusu utekelezaji wa miradi ya umeme Mkoa wa Morogoro, Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Kati, Mhandisi Aneth Malingumu amesema jumla ya Vitongoji 1,821 kati ya 3,391 tayari vimepatiwa umeme huku vitongoji 1,255 vikiwa kwenye hatua mbalimbali za kufikishiwa umeme.

 

Akiongea kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtego wa Simba Shomari Jaeka ameshukuru na kuipongeza serikali kwa kuweza kufikisha umeme katika kijiji chao na kuahidi kutumia msimu wa mavuno kuhamasisha wananchi katika kijiji chake kufanya wiring katika nyumba zao.

 

Kwa upande wake Mkandarasi anaetekeleza mradi wa HEP 2A kwa Mkoa wa Morogoro kupitia kampuni ya Sinotec, Kris Sun ameahidi watakamilisha mradi huo ndani ya muda wa mkataba.

 

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma ya umeme kwa lengo la kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Share

Print
«July 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top