Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri Ndejembi Aipongeza REA
Mohamed Saif 61

Waziri Ndejembi Aipongeza REA

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi wake hususan wa maeneo ya vijijini  kupitia Usambazaji wa Nishati ya Umeme pamoja na Nishati Safi ya Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Aprili 20, 2026 Jijini Dodoma alipotembelea Banda la REA katika Maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea ndani ya viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

"Hongereni sana wataalam mnatekeleza kwa vitendo dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wake kote nchini Nishati," amepongeza Mhe. Ndejembi

Aidha, Mhe. Ndejembi amewaalika Waheshimiwa Wabunge kutembelea Banda la Maonesho la Nishati ili kushuhudia kazi kubwa inayotekelezwa na Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zake.

"Tunawakaribisha Waheshimiwa Wabunge kutembelea Maonesho haya pamoja na wageni wao kwani ni fursa nzuri ya kukutana na wataalam na Kujadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi katika Majimbo yao," amesema Mhe. Ndejembi.

Amesema Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinashiriki na kwamba wataalam wapo tayari na ni fursa kwa Wabunge kukutana na wataalam hao ili kujadili changamoto zilizopo na kutazama namna bora ya kuzipatia ufumbuzi.

"Lengo la Maonesho haya ni kuonyesha kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuna mengi ya kujifunza kwenye banda hili," amesema Mhe. Ndejembi

Halikadhalika, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amemhakikishia Waziri Ndejembi kuwa, miradi yote inayotekelezwa kwa sasa itakamilika kwa wakati na REA imejipanga kikamilifu kutekeleza miradi hiyo. 

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni miongoni mwa Taasisi zinazoshiriki katika Maonesho hayo yaliyoanza tarehe 20 Aprili, 2026.

 

Share

Print
«June 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
12
Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.

Read more
34567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top