Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri Ndejembi Aipongeza REA
Mohamed Saif 24

Waziri Ndejembi Aipongeza REA

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi wake hususan wa maeneo ya vijijini  kupitia Usambazaji wa Nishati ya Umeme pamoja na Nishati Safi ya Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Aprili 20, 2026 Jijini Dodoma alipotembelea Banda la REA katika Maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea ndani ya viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

"Hongereni sana wataalam mnatekeleza kwa vitendo dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wake kote nchini Nishati," amepongeza Mhe. Ndejembi

Aidha, Mhe. Ndejembi amewaalika Waheshimiwa Wabunge kutembelea Banda la Maonesho la Nishati ili kushuhudia kazi kubwa inayotekelezwa na Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zake.

"Tunawakaribisha Waheshimiwa Wabunge kutembelea Maonesho haya pamoja na wageni wao kwani ni fursa nzuri ya kukutana na wataalam na Kujadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi katika Majimbo yao," amesema Mhe. Ndejembi.

Amesema Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinashiriki na kwamba wataalam wapo tayari na ni fursa kwa Wabunge kukutana na wataalam hao ili kujadili changamoto zilizopo na kutazama namna bora ya kuzipatia ufumbuzi.

"Lengo la Maonesho haya ni kuonyesha kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuna mengi ya kujifunza kwenye banda hili," amesema Mhe. Ndejembi

Halikadhalika, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amemhakikishia Waziri Ndejembi kuwa, miradi yote inayotekelezwa kwa sasa itakamilika kwa wakati na REA imejipanga kikamilifu kutekeleza miradi hiyo. 

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni miongoni mwa Taasisi zinazoshiriki katika Maonesho hayo yaliyoanza tarehe 20 Aprili, 2026.

 

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top